< Daniel 3 >
1 Nebuchadnezzar king [the] to make image that gold height his cubit sixty breadth his cubit six to stand: establish him in/on/with plain Dura in/on/with province Babylon
Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
2 and Nebuchadnezzar king [the] to send to/for to gather to/for satrap [the] prefect [the] and governor [the] judge [the] treasurer [the] judge [the] magistrate [the] and all governor province [the] to/for to come to/for dedication image [the] that to stand: establish Nebuchadnezzar king [the]
Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
3 in/on/with then to gather satrap [the] prefect [the] and governor [the] judge [the] treasurer [the] judge [the] magistrate [the] and all governor province [the] to/for dedication image [the] that to stand: establish Nebuchadnezzar king [the] (and to stand: establish *Q(k)*) to/for before image [the] that to stand: establish Nebuchadnezzar
Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
4 and proclaimer [the] to read in/on/with strength to/for you to say people [the] people [the] and tongue [the]
Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
5 in/on/with time [the] that to hear voice: sound horn [the] flute [the] (lyre *Q(k)*) trigon psaltery bagpipe and all kind music [the] to fall and to do homage to/for image gold [the] that to stand: establish Nebuchadnezzar king [the]
Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
6 and who? that not to fall and to do homage in/on/with her moment [the] to cast to/for midst furnace fire [the] to burn [the]
Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
7 like/as to/for before: because this in/on/with him time [the] like/as that to hear all people [the] voice: sound horn [the] flute [the] (lyre *Q(k)*) trigon psaltery (and bagpipe *X*) and all kind music [the] to fall all people [the] people [the] and tongue [the] to do homage to/for image gold [the] that to stand: establish Nebuchadnezzar king [the]
Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
8 like/as to/for before: because this in/on/with him time [the] to approach man Chaldean and to devour charges their that Jew [the]
Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
9 to answer and to say to/for Nebuchadnezzar king [the] king [the] to/for perpetuity to live
Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
10 (you *Q(k)*) king [the] to set: make command that all man that to hear voice: sound horn [the] flute [the] (lyre *Q(k)*) trigon psaltery (and bagpipe *Q(k)*) and all kind music [the] to fall and to do homage to/for image gold [the]
Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
11 and who? that not to fall and to do homage to cast to/for midst furnace fire [the] to burn [the]
na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
12 there is man Jew that to reckon/appoint whom them since service province Babylon Shadrach Meshach and Abednego Abednego man [the] these not to set: put/give (since you *Q(k)*) king [the] command (to/for god your *Q(K)*) not to serve and to/for image gold [the] that to stand: establish not to do homage
Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
13 in/on/with then Nebuchadnezzar in/on/with rage and rage to say to/for to come to/for Shadrach Meshach and Abednego Abednego in/on/with then man [the] these to come before king [the]
Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
14 to answer Nebuchadnezzar and to say to/for them intended Shadrach Meshach and Abednego Abednego to/for god my not there is you to serve and to/for image gold [the] that to stand: establish not to do homage
naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 now if there is you ready that in/on/with time [the] that to hear voice: sound horn [the] flute [the] (lyre *Q(k)*) trigon psaltery and bagpipe and all kind music [the] to fall and to do homage to/for image [the] that to make and if not to do homage in/on/with her moment [the] to cast to/for midst furnace fire [the] to burn [the] and who? he/she/it god that to rescue you from hand my
Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
16 to answer Shadrach Meshach and Abednego Abednego and to say to/for king [the] Nebuchadnezzar not to need we since this edict to/for to return: reply you
Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
17 if there is god our that we to serve be able to/for to rescue us from furnace fire [the] to burn [the] and from hand your king [the] to rescue
Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
18 and if not to know to be to/for you king [the] that (to/for god your *Q(K)*) not (there is we *Q(k)*) to serve and to/for image gold [the] that to stand: establish not to do homage
Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
19 in/on/with then Nebuchadnezzar to fill rage and image face his (to change *Q(K)*) since Shadrach Meshach and Abednego Abednego to answer and to say to/for to heat to/for furnace [the] one seven since that to see to/for to heat him
Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
20 and to/for man mighty strength that in/on/with strength his to say to/for to bind to/for Shadrach Meshach and Abednego Abednego to/for to cast to/for furnace fire [the] to burn [the]
na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
21 in/on/with then man [the] these to bind in/on/with mantle their (legging their *Q(k)*) and helmet their and garment their and to cast to/for midst furnace fire [the] to burn [the]
Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
22 like/as to/for before: because this from that word king [the] be hasty and furnace [the] to heat preeminent man [the] these that to take up to/for Shadrach Meshach and Abednego Abednego to slay they flame [the] that fire [the]
Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
23 and man [the] these three their Shadrach Meshach and Abednego Abednego to fall to/for midst furnace fire [the] to burn [the] to bind
Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
24 then Nebuchadnezzar king [the] be startled and to stand: rise in/on/with to dismay to answer and to say to/for counselor his not man three to cast to/for midst fire [the] to bind to answer and to say to/for king [the] certain king [the]
Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
25 to answer and to say behold me to see man four to loose to go in/on/with midst fire [the] and harm not there is in/on/with them and appearance his that (fourth [the] *Q(k)*) be like to/for son god
Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
26 in/on/with then to approach Nebuchadnezzar to/for door furnace fire [the] to burn [the] to answer and to say Shadrach Meshach and Abednego Abednego servant/slave his that god [the] (Most High [the] *Q(k)*) to go out and to come in/on/with then to go out Shadrach Meshach and Abednego Abednego from midst fire [the]
Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
27 and to gather satrap [the] prefect [the] and governor [the] and counselor king [the] to see to/for man [the] these that not to rule fire [the] in/on/with body their and hair head their not to singe and mantle their not to change and smell fire not to pass on/over/away in/on/with them
Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
28 to answer Nebuchadnezzar and to say to bless god their that Shadrach Meshach and Abednego Abednego that to send angel his and to rescue to/for servant/slave his that to trust since him and word king [the] to change and to give (body their *Q(K)*) that not to serve and not to do homage to/for all god except to/for god their
Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
29 and from me to set: make command that all people people and tongue that to say (neglect *Q(K)*) since god their that Shadrach Meshach and Abednego Abednego piece to make and house his dunghill be set like/as to/for before: because that not there is god another that be able to/for to rescue like/as this
Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
30 in/on/with then king [the] to prosper to/for Shadrach Meshach and Abednego Abednego in/on/with province Babylon
Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.