< Acts 1 >
1 the/this/who on the other hand first word to do/make: do about all oh! Theophilus which be first the/this/who Jesus to do/make: do and/both and to teach
Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2 until which day to order the/this/who apostle through/because of spirit/breath: spirit holy which to select to take up
mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 which and to stand by themself to live with/after the/this/who to suffer it/s/he in/on/among much clear proof through/because of day forty to appear it/s/he and to say the/this/who about the/this/who kingdom the/this/who God
Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4 and to assemble to order it/s/he away from Jerusalem not to separate/leave but to await the/this/who promise the/this/who father which to hear me
Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: “Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5 that/since: since John on the other hand to baptize water you then in/on/among spirit/breath: spirit to baptize holy no with/after much this/he/she/it day
Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 the/this/who on the other hand therefore/then to assemble (to ask *N(k)O*) it/s/he to say lord: God if in/on/among the/this/who time this/he/she/it to restore the/this/who kingdom the/this/who Israel
Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, “Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?”
7 to say then to/with it/s/he no you to be to know time or time/right time which the/this/who father to place in/on/among the/this/who one's own/private authority
Lakini Yesu akawaambia, “Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8 but to take power to arrive/invade the/this/who holy spirit/breath: spirit upon/to/against you and to be (me *N(K)O*) witness in/on/among and/both Jerusalem and in/on/among all the/this/who Judea and Samaria and until last/least the/this/who earth: planet
Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia.”
9 and this/he/she/it to say to see it/s/he to lift up and cloud to take up/suppose it/s/he away from the/this/who eye it/s/he
Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10 and as/when to gaze to be toward the/this/who heaven to travel it/s/he and look! man two to stand by it/s/he in/on/among (clothing white *N(k)O*)
Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11 which and to say man Galilean which? to stand (to look into/upon *NK(o)*) toward the/this/who heaven this/he/she/it the/this/who Jesus the/this/who to take up away from you toward the/this/who heaven thus(-ly) to come/go which way to look at it/s/he to travel toward the/this/who heaven
wakasema, “Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni.”
12 then to return toward Jerusalem away from mountain the/this/who to call: call Olivet which to be near Jerusalem Sabbath to have/be road
Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13 and when to enter toward the/this/who upper room to ascend whither to be to stay the/this/who and/both Peter and John and James and Andrew Philip and Thomas Bartholomew and Matthew James Alphaeus and Simon the/this/who Zealot and Judas James
Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 this/he/she/it all to be to continue in/with united the/this/who prayer (and the/this/who petition *K*) with woman and Mary the/this/who mother the/this/who Jesus and (with *ko*) the/this/who brother it/s/he
Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15 and in/on/among the/this/who day this/he/she/it to arise Peter in/on/among midst the/this/who (brother *N(K)O*) to say to be and/both crowd name upon/to/against the/this/who it/s/he (like/as/about *N(k)O*) hundred twenty
Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16 man brother be necessary to fulfill the/this/who a writing (this/he/she/it *k*) which (to foretell *NK(o)*) the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who holy through/because of mouth David about Judas the/this/who to be guide/leader the/this/who to seize/conceive/help (the/this/who *k*) Jesus
akasema, “Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17 that/since: since to number to be (in/on/among *N(k)O*) me and to choose by lot the/this/who lot the/this/who service this/he/she/it
Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18 this/he/she/it on the other hand therefore/then to posses place out from (the/this/who *k*) wage the/this/who unrighteousness and headlong to be to burst midst and to pour out all the/this/who affection/entrails it/s/he
(“Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19 and acquainted with to be all the/this/who to dwell Jerusalem so to call: call the/this/who place that the/this/who one's own/private language it/s/he Akeldama this/he/she/it to be Field (of Blood) (Field of) Blood
Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20 to write for in/on/among book psalm to be the/this/who residence it/s/he deserted and not to be the/this/who to dwell in/on/among it/s/he and the/this/who oversight it/s/he (to take *N(k)O*) other
Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21 be necessary therefore/then the/this/who to assemble me man in/on/among all time (in/on/among *k*) which to enter and to go out upon/to/against me the/this/who lord: God Jesus
Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22 be first away from the/this/who baptism John until the/this/who day which to take up away from me witness the/this/who resurrection it/s/he with me to be one this/he/she/it
Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni.”
23 and to stand two Joseph the/this/who to call: call Barsabbas which to call (on)/name Justus and Matthias
Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24 and to pray to say you lord: God heart-knower all to appoint which to select out from this/he/she/it the/this/who two one
Kisha wakasali: “Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 to take the/this/who (place *N(k)O*) the/this/who service this/he/she/it and apostleship (away from *N(k)O*) which to transgress Judas to travel toward the/this/who place the/this/who one's own/private
ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe.”
26 and to give lot (it/s/he *N(k)O*) and to collapse the/this/who lot upon/to/against Matthias and to numbered with with/after the/this/who eleven apostle
Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.