< Acts 28 >
1 and to save then (to come to know *N(K)O*) that/since: that Malta the/this/who island to call: call
Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2 the/this/who (and/both *N(k)O*) barbarian to furnish occasion no the/this/who to obtain/happen benevolence me (to touch *N(k)O*) for fire to take all me through/because of the/this/who rain the/this/who to approach and through/because of the/this/who cold
Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3 to gather then the/this/who Paul brushwood (one *no*) multitude and to put/lay on upon/to/against the/this/who fire snake (away from *N(k)O*) the/this/who heat to go out to attach the/this/who hand it/s/he
Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4 as/when then to perceive: see the/this/who barbarian to hang the/this/who wild animal out from the/this/who hand it/s/he to/with one another to say surely murderer to be the/this/who a human this/he/she/it which to save out from the/this/who sea the/this/who condemnation to live no to allow
Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, “Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!”
5 the/this/who on the other hand therefore/then (to shake off *NK(o)*) the/this/who wild animal toward the/this/who fire to suffer none evil/harm: harm
Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6 the/this/who then to look for it/s/he to ensue to swell up or to fall down suddenly dead upon/to/against much then it/s/he to look for and to see/experience nothing wrong toward it/s/he to be (to change mind *N(k)O*) to say it/s/he to exist God
Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7 in/on/among then the/this/who about the/this/who place that be already place the/this/who first: chief the/this/who island name Publius which to receive me Three day hospitably to host
Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8 to be then the/this/who father the/this/who Publius fever and (dysentery *N(k)O*) to hold/oppress to recline to/with which the/this/who Paul to enter and to pray to put/lay on the/this/who hand it/s/he to heal it/s/he
Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9 this/he/she/it (then *N(k)O*) to be and the/this/who remaining the/this/who in/on/among the/this/who island to have/be weakness: ill to come near/agree and to serve/heal
Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10 which and much honor to honor me and to lead to put/lay on the/this/who to/with (the/this/who need *N(k)O*)
Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11 with/after then Three month (to lead *NK(o)*) in/on/among boat to winter in/on/among the/this/who island Alexandria figurehead the twin gods
Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo “Miungu Pacha”. Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12 and to bring down toward Syracuse to remain/keep on day Three
Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13 whence (to take away *N(K)O*) to come to toward Rhegium and with/after one day to arise/spring up south the next day to come/go toward Puteoli
Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14 whither to find/meet brother to plead/comfort (from/with/beside *N(k)O*) it/s/he to remain/keep on day seven and thus(-ly) toward the/this/who Rome to come/go
Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15 and from there the/this/who brother to hear the/this/who about me (to come/go *N(k)O*) toward meeting me until of Appius Forum and Three Taverns which to perceive: see the/this/who Paul to thank the/this/who God to take courage/confidence
Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16 when then (to enter *N(k)O*) toward Rome (the/this/who centurion to deliver the/this/who prisoner the/this/who commander *K*) to permit the/this/who (then *k*) Paul to stay according to themself with the/this/who to keep/guard: guard it/s/he soldier
Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17 to be then with/after day Three to call together (the/this/who *k*) (it/s/he *N(K)O*) the/this/who to be the/this/who Jew first: chief to assemble then it/s/he to say to/with it/s/he I/we man brother none hostile to do/make: do the/this/who a people or the/this/who custom the/this/who ancestral prisoner out from Jerusalem to deliver toward the/this/who hand the/this/who Roman
Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, “Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18 who/which to investigate me to plan to release: release through/because of the/this/who nothing cause/charge death be already in/on/among I/we
Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19 to dispute then the/this/who Jew to compel to call (on)/name Caesar no as/when the/this/who Gentiles me to have/be one (to accuse *N(k)O*)
Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20 through/because of this/he/she/it therefore/then the/this/who cause/charge to plead/comfort you to perceive: see and to talk to/with because of for the/this/who hope the/this/who Israel the/this/who chain this/he/she/it to surround
Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli.”
21 the/this/who then to/with it/s/he to say me neither something written about you to receive away from the/this/who Judea neither to come one the/this/who brother to announce or to speak one about you evil/bad
Wao wakamwambia, “Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22 to deem worthy then from/with/beside you to hear which to reason about on the other hand for the/this/who sect this/he/she/it acquainted with me to be that/since: that everywhere to dispute
Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali.”
23 to appoint then it/s/he day (to come/go *N(k)O*) to/with it/s/he toward the/this/who lodging greater which to explain/expose to testify solemnly the/this/who kingdom the/this/who God to persuade and/both it/s/he (the/this/who *k*) about the/this/who Jesus away from and/both the/this/who law Moses and the/this/who prophet away from early until evening
Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24 and the/this/who on the other hand to persuade the/this/who to say the/this/who then to disbelieve
Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25 discordant then to be to/with one another to release: release to say the/this/who Paul declaration one that/since: that well the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who holy to speak through/because of Isaiah the/this/who prophet to/with the/this/who father (you *N(K)O*)
Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, “Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26 (to say *N(k)O*) to travel to/with the/this/who a people this/he/she/it and to say hearing to hear and no not to understand and to see to see and no not to perceive: understand
akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27 to thicken for the/this/who heart the/this/who a people this/he/she/it and the/this/who ear difficultly to hear and the/this/who eye it/s/he to close not once/when to perceive: see the/this/who eye and the/this/who ear to hear and the/this/who heart to understand and to turn and (to heal *N(k)O*) it/s/he
Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.”
28 acquainted with therefore/then to be you that/since: that the/this/who Gentiles to send (this/he/she/it *no*) the/this/who salvation the/this/who God it/s/he and to hear
Halafu Paulo akamaliza na kusema, “Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!”
29 (and this/he/she/it it/s/he to say to go away the/this/who Jew much to have/be in/on/among themself discussion *K*)
Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30 (to abide in/by *N(k)O*) then (the/this/who Paul *k*) two years all in/on/among one's own/private rented home and to receive all the/this/who to enter to/with it/s/he
Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31 to preach the/this/who kingdom the/this/who God and to teach the/this/who about the/this/who lord: God Jesus Christ with/after all boldness freely
Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.