< Acts 27 >

1 as/when then to judge the/this/who to set sail me toward the/this/who Italy to deliver the/this/who and/both Paul and one other prisoner centurion name Julius band Augustan
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 to mount/board then boat Adramyttium (to ensue *N(k)O*) to sail (toward *no*) the/this/who according to the/this/who Asia place to lead to be with me Aristarchus Macedonia Thessalonian
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 the/this/who and/both other to bring down toward Sidon benevolently and/both the/this/who Julius the/this/who Paul to use to permit to/with the/this/who friendly/friend (to travel *N(k)O*) care to obtain/happen
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 and from there to lead to sail the lee the/this/who Cyprus through/because of the/this/who the/this/who wind to exist hostile
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 the/this/who and/both sea the/this/who according to the/this/who Cilicia and Pamphylia to sail across to descend toward Myra the/this/who Lycia
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 and there to find/meet the/this/who centurion boat Alexandria to sail toward the/this/who Italy to put on board me toward it/s/he
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 in/on/among sufficient then day to sail slowly and hardly to be according to the/this/who Cnidus not to permit me the/this/who wind to sail the lee the/this/who Crete according to Salmone
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 hardly and/both to sail past it/s/he to come/go toward place one to call: call Fair (Havens) Havens which near city to be Lasea
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 sufficient then time to pass and to be already dangerous/unsteady the/this/who voyage through/because of the/this/who and the/this/who fasting already to pass by to urge the/this/who Paul
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 to say it/s/he man to see/experience that/since: that with/after mistreatment and much damage/loss no alone the/this/who (burden *N(k)O*) and the/this/who boat but and the/this/who soul: life me to ensue to be the/this/who voyage
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 the/this/who then centurion the/this/who captain and the/this/who captain more to persuade or the/this/who by/under: by (the/this/who *k*) Paul to say
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 unsuitable then the/this/who Havens be already to/with wintering the/this/who greater to place plan to lead (from there *N(k)O*) if how be able to come to toward Phoenix to winter Havens the/this/who Crete to see according to southwest and according to northwest
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 to blow gently then south to think the/this/who purpose to grasp/seize to take up nearer to sail past the/this/who Crete
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 with/after no much then to throw: throw according to it/s/he wind tempestuous the/this/who to call: call a north wind
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 to seize then the/this/who boat and not be able to face the/this/who wind to give/deliver to bear/lead
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 small island then one to sail under to call: call (Cauda *N(K)O*) be strong hardly in control of to be the/this/who lifeboat
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 which to take up help to use to undergird the/this/who boat to fear and/both not toward the/this/who Syrtis to fall out to lower the/this/who vessel thus(-ly) to bear/lead
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 violently then be storm-tossed me the/this/who next/afterward jettisoning to do/make: do
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 and the/this/who third with one’s own hand the/this/who gear the/this/who boat (to throw/lay down *N(K)O*)
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 neither then sun neither star to appear upon/to/against greater day winter and/both no little/few to lay on henceforth to take away hope all the/this/who to save me
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 much (and/both *N(k)O*) fasting be already then to stand the/this/who Paul in/on/among midst it/s/he to say be necessary on the other hand oh! man to obey me not to lead away from the/this/who Crete to gain and/both the/this/who mistreatment this/he/she/it and the/this/who damage/loss
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 and the/this/who now to urge you be cheerful deprivation for soul: life none to be out from you but/however the/this/who boat
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 to stand by for me this/he/she/it the/this/who night the/this/who God which to be (I/we *n*) which and to minister angel
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 to say not to fear Paul Caesar you be necessary to stand by and look! to give grace you the/this/who God all the/this/who to sail with/after you
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 therefore be cheerful man to trust (in) for the/this/who God that/since: that thus(-ly) to be according to which way to speak me
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 toward island then one be necessary me to fall out
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 as/when then fourteenth night to be to spread/surpass me in/on/among the/this/who Adriatic Sea according to midst the/this/who night to suppose the/this/who sailor to bring near one it/s/he country
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 and to sound to find/meet a fathom twenty little then to pass and again to sound to find/meet a fathom fifteen
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 to fear and/both not how (according to *N(k)O*) rough place (to fall out *NK(O)*) out from stern to throw/lay down anchor four to pray/wish for day to be
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 the/this/who then sailor to seek to flee out from the/this/who boat and to lower the/this/who lifeboat toward the/this/who sea pretense as/when out from bow anchor to ensue to stretch out
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 to say the/this/who Paul the/this/who centurion and the/this/who soldier if not this/he/she/it to stay in/on/among the/this/who boat you to save no be able
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 then to cut off the/this/who soldier the/this/who rope the/this/who lifeboat and to allow it/s/he to fall out
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 until then which day to ensue to be to plead/comfort the/this/who Paul all to partake food to say fourteenth today day to look for fasting to continue nothing to take
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 therefore to plead/comfort you (to partake *N(k)O*) food this/he/she/it for to/with the/this/who you salvation be already none for you hair (away from *N(k)O*) the/this/who head (to destroy *N(K)O*)
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 to say then this/he/she/it and to take bread to thank the/this/who God before all and to break be first to eat
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 encouraging then to be all and it/s/he to take food
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 (to be *N(k)O*) then the/this/who all soul: person in/on/among the/this/who boat (two hundred *NK(O)*) seventy six
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 to satisfy then (the/this/who *o*) food to lighten the/this/who boat to expel the/this/who grain toward the/this/who sea
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 when then day to be the/this/who earth: country no to come to know bosom then one to observe to have/be shore toward which (to plan *N(k)O*) if (be able *NK(o)*) (to expel *NK(O)*) the/this/who boat
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 and the/this/who anchor to take away to allow toward the/this/who sea together to loosen/leave the/this/who rope the/this/who rudder and to lift up the/this/who foresail the/this/who to blow to hold back/fast toward the/this/who shore
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 to fall upon then toward place sandbar to run aground the/this/who ship and the/this/who on the other hand bow to immobilise to stay unshakable the/this/who then stern to loose by/under: by the/this/who force the/this/who a wave
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 the/this/who then soldier plan to be in order that/to the/this/who prisoner to kill not one to swim out (to escape *N(k)O*)
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 the/this/who then centurion to plan to save the/this/who Paul to prevent it/s/he the/this/who plan to order and/both the/this/who be able to swim to throw off first upon/to/against the/this/who earth: country to go out/away
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 and the/this/who remaining which on the other hand upon/to/against plank which then upon/to/against one the/this/who away from the/this/who boat and thus(-ly) to be all to save upon/to/against the/this/who earth: country
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.

< Acts 27 >