< 2 Samuel 23 >
1 and these word David [the] last utterance David son: child Jesse and utterance [the] great man to arise: raise height anointed God Jacob and musical song Israel
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 spirit LORD to speak: speak in/on/with me and speech his upon tongue my
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 to say God Israel to/for me to speak: speak rock Israel to rule in/on/with man righteous to rule fear God
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 and like/as light morning to rise sun morning not cloud from brightness from rain grass from land: soil
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 for not so house: household my with God for covenant forever: enduring to set: make to/for me to arrange in/on/with all and to keep: guard for all salvation my and all pleasure for not to spring
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 and Belial like/as thorn to wander all their for not in/on/with hand to take: take
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 and man: anyone to touch in/on/with them to fill iron and tree: stake spear and in/on/with fire to burn to burn in/on/with seat
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 these name [the] mighty man which to/for David Josheb-basshebeth Josheb-basshebeth Tahchemonite head: leader [the] officer he/she/it `wielded` ([the] Eznite *Q(K)*) upon eight hundred slain: killed in/on/with beat (one *Q(K)*)
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 (and after him *Q(k)*) Eleazar son: child (Dodo *Q(K)*) son: child Ahohite in/on/with three ([the] mighty man *Q(K)*) with David in/on/with to taunt they in/on/with Philistine to gather there to/for battle and to ascend: rise man Israel
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 he/she/it to arise: rise and to smite in/on/with Philistine till for be weary/toil hand: power his and to cleave hand: power his to(wards) [the] sword and to make: do LORD deliverance: victory great: large in/on/with day [the] he/she/it and [the] people: soldiers to return: return after him surely to/for to strip
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 and after him Shammah son: child Agee Hararite and to gather Philistine to/for community and to be there portion [the] land: soil full lentil and [the] people: soldiers to flee from face: before Philistine
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 and to stand in/on/with midst [the] portion and to rescue her and to smite [obj] Philistine and to make: do LORD deliverance: victory great: large
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 and to go down (three *Q(K)*) from [the] thirty head: leader and to come (in): come to(wards) harvest to(wards) David to(wards) cave Adullam and community Philistine to camp in/on/with Valley (of Rephaim) (Valley of) Rephaim
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 and David then in/on/with fortress and station Philistine then Bethlehem Bethlehem
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 and to desire David and to say who? to water: drink me water from cistern Bethlehem Bethlehem which in/on/with gate
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 and to break up/open three [the] mighty man in/on/with camp Philistine and to draw water from cistern Bethlehem Bethlehem which in/on/with gate and to lift: bear and to come (in): bring to(wards) David and not be willing to/for to drink them and to pour [obj] them to/for LORD
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 and to say forbid to/for me LORD from to make: do I this blood [the] human [the] to go: went in/on/with soul: life their and not be willing to/for to drink them these to make: do three [the] mighty man
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 and Abishai brother: male-sibling Joab son: child Zeruiah he/she/it head: leader ([the] three *Q(K)*) and he/she/it to rouse [obj] spear his upon three hundred slain: killed and to/for him name in/on/with three
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 from [the] three for to honor: honour and to be to/for them to/for ruler and till [the] three not to come (in): come
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 and Benaiah son: child Jehoiada son: warrior man (strength *Q(K)*) many work from Kabzeel he/she/it to smite [obj] two Ariel Moab and he/she/it to go down and to smite [obj] ([the] lion *Q(K)*) in/on/with midst [the] pit in/on/with day [the] snow
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 and he/she/it to smite [obj] man Egyptian (man *Q(K)*) appearance and in/on/with hand [the] Egyptian spear and to go down to(wards) him in/on/with tribe: staff and to plunder [obj] [the] spear from hand [the] Egyptian and to kill him in/on/with spear his
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 these to make: do Benaiah son: child Jehoiada and to/for him name in/on/with three [the] mighty man
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 from [the] thirty to honor: honour and to(wards) [the] three not to come (in): come and to set: appoint him David to(wards) guard his
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Asahel Asahel brother: male-sibling Joab in/on/with thirty Elhanan son: child Dodo Bethlehem Bethlehem
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 Shammah [the] Harodite Elika [the] Harodite
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Helez [the] Paltite Ira son: child Ikkesh [the] Tekoa
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Abiezer [the] Anathoth Mebunnai [the] Hushathite
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Zalmon [the] Ahohite Maharai [the] Netophathite
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Heleb son: child Baanah [the] Netophathite Ittai son: child Ribai from Gibeah son: descendant/people Benjamin
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Benaiah Pirathon Hiddai from torrent: river Gaash
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Abi-albon Abi-albon [the] Arbathite Azmaveth [the] Bahurite
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Eliahba [the] Shaalbonite son: child Jashen Jonathan
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 (son: child *X*) Shammah [the] Hararite Ahiam son: child Sharar [the] Hararite
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Eliphelet son: child Ahasbai son: child [the] Maacathite Eliam son: child Ahithophel [the] Gilonite
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 (Hezro *Q(K)*) [the] Carmelite Paarai [the] Arbite
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Igal son: child Nathan from Zobah Bani [the] Gad
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Zelek [the] Ammon Naharai [the] Beerothite (to lift: bearing(armour) *Q(K)*) article/utensil Joab son: child Zeruiah
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Ira [the] Ithrite Gareb [the] Ithrite
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Uriah [the] Hittite all thirty and seven
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.