< 2 Kings 7 >

1 and to say Elisha to hear: hear word LORD thus to say LORD like/as time tomorrow seah fine flour in/on/with shekel and seah barley in/on/with shekel in/on/with gate Samaria
Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
2 and to answer [the] officer which to/for king to lean upon hand his [obj] man [the] God and to say behold LORD to make window in/on/with heaven to be [the] word: thing [the] this and to say look! you to see: see in/on/with eye your and from there not to eat
Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
3 and four human to be be leprous entrance [the] gate and to say man: anyone to(wards) neighbor his what? we to dwell here till to die
Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
4 if to say to come (in): come [the] city and [the] famine in/on/with city and to die there and if to dwell here and to die and now to go: come! and to fall: fall to(wards) camp Syria if to live us to live and if to die us and to die
Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
5 and to arise: rise in/on/with twilight to/for to come (in): come to(wards) camp Syria and to come (in): come till end camp Syria and behold nothing there man: anyone
Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
6 and Lord to hear: hear [obj] camp Syria voice: sound chariot voice: sound horse voice: sound strength: soldiers great: large and to say man: anyone to(wards) brother: compatriot his behold to hire upon us king Israel [obj] king [the] Hittite and [obj] king Egypt to/for to come (in): come upon us
kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
7 and to arise: rise and to flee in/on/with twilight and to leave: forsake [obj] tent their and [obj] horse their and [obj] donkey their [the] camp like/as as which he/she/it and to flee to(wards) soul: life their
Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
8 and to come (in): come [the] be leprous [the] these till end [the] camp and to come (in): come to(wards) tent one and to eat and to drink and to lift: bear from there silver: money and gold and garment and to go: went and to hide and to return: return and to come (in): come to(wards) tent another and to lift: bear from there and to go: went and to hide
Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
9 and to say man: anyone to(wards) neighbor his not right we to make: do [the] day: today [the] this day: today good news he/she/it and we be silent and to wait till light [the] morning and to find us iniquity: punishment and now to go: come! and to come (in): come and to tell house: household [the] king
Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
10 and to come (in): come and to call: call to to(wards) gatekeeper [the] city and to tell to/for them to/for to say to come (in): come to(wards) camp Syria and behold nothing there man: anyone and voice: listen man that if: except if: except [the] horse to bind and [the] donkey to bind and tent like/as as which they(masc.)
Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
11 and to call: call to [the] gatekeeper and to tell house: household [the] king within
Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
12 and to arise: rise [the] king night and to say to(wards) servant/slave his to tell please to/for you [obj] which to make: do to/for us Syria to know for hungry we and to come out: come from [the] camp to/for to hide (in/on/with land: country *Q(K)*) to/for to say for to come out: come from [the] city and to capture them alive and to(wards) [the] city to come (in): come
Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
13 and to answer one from servant/slave his and to say and to take: take please five from [the] horse [the] to remain which to remain in/on/with her behold they like/as all (crowd *Q(K)*) Israel which to remain in/on/with her look! they like/as all crowd Israel which to finish and to send: depart and to see: see
Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
14 and to take: take two chariot horse and to send: depart [the] king after camp Syria to/for to say to go: went and to see: see
Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
15 and to go: follow after them till [the] Jordan and behold all [the] way: road full garment and article/utensil which to throw Syria (in/on/with to hurry they *Q(K)*) and to return: return [the] messenger and to tell to/for king
Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
16 and to come out: come [the] people and to plunder [obj] camp Syria and to be seah fine flour in/on/with shekel and seah barley in/on/with shekel like/as word LORD
Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
17 and [the] king to reckon: overseer [obj] [the] officer which to lean upon hand: power his upon [the] gate and to trample him [the] people in/on/with gate and to die like/as as which to speak: speak man [the] God which to speak: speak in/on/with to go down [the] king to(wards) him
Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
18 and to be like/as to speak: speak man [the] God to(wards) [the] king to/for to say seah barley in/on/with shekel and seah fine flour in/on/with shekel to be like/as time tomorrow in/on/with gate Samaria
Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
19 and to answer [the] officer [obj] man [the] God and to say and behold LORD to make window in/on/with heaven to be like/as Chronicles [the] this and to say look! you to see: see in/on/with eye your and from there not to eat
Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
20 and to be to/for him so and to trample [obj] him [the] people in/on/with gate and to die
Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.

< 2 Kings 7 >