< 2 Chronicles 31 >

1 and like/as to end: finish all this to come out: come all Israel [the] to find to/for city Judah and to break [the] pillar and to cut down/off [the] Asherah and to tear [obj] [the] high place and [obj] [the] altar from all Judah and Benjamin and in/on/with Ephraim and Manasseh till to/for to end: destroy and to return: return all son: descendant/people Israel man: anyone to/for possession his to/for city their
Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
2 and to stand: appoint Hezekiah [obj] division [the] priest and [the] Levi upon division their man: anyone like/as lip: according service: ministry his to/for priest and to/for Levi to/for burnt offering and to/for peace offering to/for to minister and to/for to give thanks and to/for to boast: praise in/on/with gate camp LORD
Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
3 and portion [the] king from property his to/for burnt offering to/for burnt offering [the] morning and [the] evening and [the] burnt offering to/for Sabbath and to/for month: new moon and to/for meeting: festival like/as to write in/on/with instruction LORD
Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
4 and to say to/for people to/for to dwell Jerusalem to/for to give: give portion [the] priest and [the] Levi because to strengthen: strengthen in/on/with instruction LORD
Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
5 and like/as to break through [the] word to multiply son: descendant/people Israel first: beginning grain new wine and oil and honey and all produce land: country and tithe [the] all to/for abundance to come (in): bring
Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
6 and son: descendant/people Israel and Judah [the] to dwell in/on/with city Judah also they(masc.) tithe cattle and flock and tithe holiness [the] to consecrate: dedicate to/for LORD God their to come (in): bring and to give: put heap heap
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
7 in/on/with month [the] third to profane/begin: begin [the] heap to/for to found and in/on/with month [the] seventh to end: finish
Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
8 and to come (in): come Hezekiah and [the] ruler and to see: see [obj] [the] heap and to bless [obj] LORD and [obj] people his Israel
Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
9 and to seek Hezekiah upon [the] priest and [the] Levi upon [the] heap
Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
10 and to say to(wards) him Azariah [the] priest [the] head: leader to/for house: home Zadok and to say from to profane/begin: begin [the] contribution to/for to come (in): bring house: temple LORD to eat and to satisfy and to remain till to/for abundance for LORD to bless [obj] people his and [the] to remain [obj] [the] crowd [the] this
naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
11 and to say Hezekiah to/for to establish: prepare chamber in/on/with house: temple LORD and to establish: prepare
Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
12 and to come (in): bring [obj] [the] contribution and [the] tithe and [the] holiness in/on/with faithfulness and upon them leader (Conaniah *Q(k)*) [the] Levi and Shimei brother: male-sibling his second
Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
13 and Jehiel and Azaziah and Nahath and Asahel and Jerimoth and Jozabad and Eliel and Ismachiah and Mahath and Benaiah overseer from hand (Conaniah *Q(k)*) and Shimei brother: male-sibling his in/on/with appointment Hezekiah [the] king and Azariah leader house: temple [the] God
Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
14 and Kore son: child Imnah [the] Levi [the] gatekeeper to/for east [to] upon voluntariness [the] God to/for to give: put contribution LORD and holiness [the] holiness
Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
15 and upon hand his Eden and Miniamin and Jeshua and Shemaiah Amariah and Shecaniah in/on/with city [the] priest in/on/with faithfulness to/for to give: give to/for brother: male-relative their in/on/with division like/as great: large like/as small
Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 from to/for alone: besides to enroll they to/for male from son: aged three year and to/for above [to] to/for all [the] to come (in): come to/for house: temple LORD to/for word: promised day: daily in/on/with day: daily his to/for service: ministry their in/on/with charge their like/as division their
Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
17 and [obj] genealogy [the] priest to/for house: household father their and [the] Levi from son: aged twenty year and to/for above [to] in/on/with charge their in/on/with division their
Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
18 and to/for genealogy in/on/with all child their woman: wife their and son: child their and daughter their to/for all assembly for in/on/with faithfulness their to consecrate: consecate holiness
Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
19 and to/for son: descendant/people Aaron [the] priest in/on/with land: country pasture city their in/on/with all city and city human which to pierce in/on/with name to/for to give: give portion to/for all male in/on/with priest and to/for all to enroll in/on/with Levi
Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
20 and to make: do like/as this Hezekiah in/on/with all Judah and to make: do [the] pleasant and [the] upright and [the] truth: faithful to/for face: before LORD God his
Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
21 and in/on/with all deed: work which to profane/begin: begin in/on/with service: ministry house: temple [the] God and in/on/with instruction and in/on/with commandment to/for to seek to/for God his in/on/with all heart his to make: do and to prosper
Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

< 2 Chronicles 31 >