< 2 Chronicles 20 >

1 and to be after so to come (in): come son: descendant/people Moab and son: descendant/people Ammon and with them from [the] Meunite upon Jehoshaphat to/for battle
Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
2 and to come (in): come and to tell to/for Jehoshaphat to/for to say to come (in): come upon you crowd many from side: beyond to/for sea from Edom and behold they in/on/with Hazazon-tamar Hazazon-tamar he/she/it Engedi Engedi
Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
3 and to fear and to give: put Jehoshaphat [obj] face his to/for to seek to/for LORD and to call: call out fast upon all Judah
Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
4 and to gather Judah to/for to seek from LORD also from all city Judah to come (in): come to/for to seek [obj] LORD
Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
5 and to stand: stand Jehoshaphat in/on/with assembly Judah and Jerusalem in/on/with house: temple LORD to/for face: before [the] court [the] new
Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
6 and to say LORD God father our not you(m. s.) he/she/it God in/on/with heaven and you(m. s.) to rule in/on/with all kingdom [the] nation and in/on/with hand: power your strength and might and nothing with you to/for to stand
akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
7 not you(m. s.) God our to possess: take [obj] to dwell [the] land: country/planet [the] this from to/for face: before people your Israel and to give: give her to/for seed: children Abraham to love: friend you to/for forever: enduring
Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
8 and to dwell in/on/with her and to build to/for you in/on/with her sanctuary to/for name your to/for to say
Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
9 if to come (in): come upon us distress: harm sword judgment and pestilence and famine to stand: stand to/for face: before [the] house: home [the] this and to/for face: before your for name your in/on/with house: home [the] this and to cry out to(wards) you from distress our and to hear: hear and to save
‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
10 and now behold son: descendant/people Ammon and Moab and mountain: mount (Mount) Seir which not to give: allow to/for Israel to/for to come (in): come in/on/with them in/on/with to come (in): come they from land: country/planet Egypt for to turn aside: turn aside from upon them and not to destroy them
“Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
11 and behold they(masc.) to wean upon us to/for to come (in): come to/for to drive out: drive out us from possession your which to possess: possess us
tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
12 God our not to judge in/on/with them for nothing in/on/with us strength to/for face: before [the] crowd [the] many [the] this [the] to come (in): come upon us and we not to know what? to make: do for upon you eye our
Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
13 (and all *LAB(h)*) Judah to stand: stand to/for face: before LORD also child their woman: wife their and son: child their
Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
14 and Jahaziel son: descendant/people Zechariah son: descendant/people Benaiah son: descendant/people Jeiel son: descendant/people Mattaniah [the] Levi from son: descendant/people Asaph to be upon him spirit LORD in/on/with midst [the] assembly
Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
15 and to say to listen all Judah and to dwell Jerusalem and [the] king Jehoshaphat thus to say LORD to/for you you(m. p.) not to fear and not to to be dismayed from face: because [the] crowd [the] many [the] this for not to/for you [the] battle for to/for God
Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
16 tomorrow to go down upon them look! they to ascend: rise in/on/with ascent [the] Ziz and to find [obj] them in/on/with end [the] torrent: valley face: east wilderness Jeruel
Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
17 not to/for you to/for to fight in/on/with this to stand to stand: stand and to see: see [obj] salvation LORD with you Judah and Jerusalem not to fear and not to to be dismayed tomorrow to come out: come to/for face: before their and LORD with you
Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
18 and to bow Jehoshaphat face land: soil [to] and all Judah and to dwell Jerusalem to fall: fall to/for face: before LORD to/for to bow to/for LORD
Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
19 and to arise: rise [the] Levi from son: descendant/people [the] Kohathite and from son: descendant/people [the] Korahite to/for to boast: praise to/for LORD God Israel in/on/with voice great: large to/for above [to]
Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
20 and to rise in/on/with morning and to come out: come to/for wilderness Tekoa and in/on/with to come out: come they to stand: stand Jehoshaphat and to say to hear: hear me Judah and to dwell Jerusalem be faithful in/on/with LORD God your and be faithful be faithful in/on/with prophet his and to prosper
Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
21 and to advise to(wards) [the] people and to stand: appoint to sing to/for LORD and to boast: praise to/for adornment holiness in/on/with to come out: come to/for face: before [the] to arm and to say to give thanks to/for LORD for to/for forever: enduring kindness his
Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
22 and in/on/with time to profane/begin: begin in/on/with cry and praise to give: put LORD to ambush upon son: descendant/people Ammon Moab and mountain: mount (Mount) Seir [the] to come (in): come to/for Judah and to strike
Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
23 and to stand: rise son: descendant/people Ammon and Moab upon to dwell mountain: mount (Mount) Seir to/for to devote/destroy and to/for to destroy and like/as to end: finish they in/on/with to dwell (Mount) Seir to help man: anyone in/on/with neighbor his to/for destruction
Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
24 and Judah to come (in): come upon [the] lookout to/for wilderness and to turn to(wards) [the] crowd and look! they corpse to fall: fall land: soil [to] and nothing survivor
Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
25 and to come (in): come Jehoshaphat and people his to/for to plunder [obj] spoil their and to find in/on/with them to/for abundance and property and corpse and article/utensil precious thing and to rescue to/for them to/for nothing burden and to be day three to plunder [obj] [the] spoil for many he/she/it
Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
26 and in/on/with day: today [the] fourth to gather to/for Valley (of Beracah) Beracah (Valley) for there to bless [obj] LORD upon so to call: call by [obj] name [the] place [the] he/she/it Valley (of Beracah) Beracah (Valley) till [the] day: today
Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
27 and to return: return all man Judah and Jerusalem and Jehoshaphat in/on/with head: leader their to/for to return: return to(wards) Jerusalem in/on/with joy for to rejoice them LORD from enemy their
Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
28 and to come (in): come Jerusalem in/on/with harp and in/on/with lyre and in/on/with trumpet to(wards) house: temple LORD
Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
29 and to be dread God upon all kingdom [the] land: country/planet in/on/with to hear: hear they for to fight LORD with enemy Israel
Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
30 and to quiet royalty Jehoshaphat and to rest to/for him God his from around
Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
31 and to reign Jehoshaphat upon Judah son: aged thirty and five year in/on/with to reign he and twenty and five year to reign in/on/with Jerusalem and name mother his Azubah daughter Shilhi
Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
32 and to go: walk in/on/with way: conduct father his Asa and not to turn aside: turn aside from her to/for to make: do [the] upright in/on/with eye: seeing LORD
Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
33 surely [the] high place not to turn aside: remove and still [the] people not to establish: establish heart their to/for God father their
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
34 and remainder word: deed Jehoshaphat [the] first and [the] last look! they to write in/on/with word: deed Jehu son: child Hanani which to ascend: establish upon scroll: book king Israel
Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
35 and after so to unite Jehoshaphat king Judah with Ahaziah king Israel he/she/it be wicked to/for to make: do
Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
36 and to unite him with him to/for to make fleet to/for to go: went Tarshish and to make fleet in/on/with Ezion-geber Ezion-geber
Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
37 and to prophesy Eliezer son: child Dodavahu from Mareshah upon Jehoshaphat to/for to say like/as to unite you with Ahaziah to break through LORD [obj] deed: work your and to break fleet and not to restrain to/for to go: went to(wards) Tarshish
Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.

< 2 Chronicles 20 >