< 1 Samuel 24 >
1 and to be like/as as which to return: return Saul from after Philistine and to tell to/for him to/for to say behold David in/on/with wilderness Engedi Engedi
Baada ya Sauli kurudi kuwafuatia Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika Jangwa la En-Gedi.”
2 and to take: take Saul three thousand man to choose from all Israel and to go: went to/for to seek [obj] David and human his upon face: before Rocks (of Goats) [the] Wildgoats'
Basi Sauli akachukua watu hodari 3,000 kutoka Israeli yote kwenda kumsaka Daudi na watu wake karibu na Majabali ya Mbuzi-Mwitu.
3 and to come (in): come to(wards) wall [the] flock upon [the] way: road and there cave and to come (in): come Saul to/for to cover [obj] foot his and David and human his in/on/with flank [the] cave to dwell
Akaja mpaka kwenye mazizi ya kondoo kando ya njia, hapo palikuwa na pango, na Sauli akaingia ndani kujipumzisha. Daudi na watu wake walikuwa wamo mle pangoni kwa ndani zaidi.
4 and to say human David to(wards) him behold [the] day which to say LORD to(wards) you behold I to give: give [obj] (enemy your *Q(K)*) in/on/with hand: power your and to make: do to/for him like/as as which be good in/on/with eye: appearance your and to arise: rise David and to cut: eliminate [obj] wing [the] robe which to/for Saul in/on/with secrecy
Watu wa Daudi wakasema, “Hii ndiyo siku aliyonena Bwana akikuambia, ‘Nitamtia adui yako mikononi mwako ili wewe umtendee utakavyo.’” Basi Daudi akanyemelea bila kuonekana na kukata upindo wa joho la Sauli.
5 and to be after so and to smite heart David [obj] him upon which to cut: eliminate [obj] wing which to/for Saul
Baada ya hilo, dhamiri ya Daudi ikataabika kwa kukata upindo wa joho la Sauli.
6 and to say to/for human his forbid to/for me from LORD if: surely no to make: do [obj] [the] word: thing [the] this to/for lord my to/for anointed LORD to/for to send: reach hand my in/on/with him for anointed LORD he/she/it
Akawaambia watu wake, “Bwana na apishie mbali nisije nikafanya jambo kama hilo kwa bwana wangu, yeye ambaye ni mpakwa mafuta wa Bwana, au kuinua mkono wangu dhidi yake; kwani yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.”
7 and to cleave David [obj] human his in/on/with word and not to give: allow them to/for to arise: attack to(wards) Saul and Saul to arise: rise from [the] cave and to go: went in/on/with way: journey
Kwa maneno haya Daudi akawaonya watu wake na hakuwaruhusu wamshambulie Sauli. Naye Sauli akaondoka pangoni na kwenda zake.
8 and to arise: rise David after so and to come out: come (from from [the] cave *Q(K)*) and to call: call out after Saul to/for to say lord my [the] king and to look Saul after him and to bow David face land: soil [to] and to bow
Ndipo Daudi naye akatoka pangoni na kumwita Sauli akisema, “Mfalme, bwana wangu!” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama na kusujudu uso wake mpaka nchi.
9 and to say David to/for Saul to/for what? to hear: hear [obj] word man to/for to say behold David to seek distress: harm your
Akamwambia Sauli, “Kwa nini unasikiliza wakati watu wanapokuambia, ‘Daudi amenuia kukudhuru’?
10 behold [the] day: today [the] this to see: see eye your [obj] which to give: give you LORD [the] day: today in/on/with hand my in/on/with cave and to say to/for to kill you and to pity upon you and to say not to send: reach hand my in/on/with lord my for anointed LORD he/she/it
Leo umeona kwa macho yako mwenyewe jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu huko pangoni. Watu wengine walisisitiza nikuue, lakini nilikuacha, nikisema, ‘Sitainua mkono wangu dhidi ya bwana wangu, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.’
11 and father my to see: behold! also to see: behold! [obj] wing robe your in/on/with hand: power my for in/on/with to cut: cut I [obj] wing robe your and not to kill you to know and to see: behold! for nothing in/on/with hand my distress: evil and transgression and not to sin to/for you and you(m. s.) to ambush [obj] soul: life my to/for to take: take her
Tazama, baba yangu, ona kipande hiki cha joho lako mkononi mwangu! Nilikata upindo wa joho lako lakini sikukuua. Basi ujue na kutambua kuwa sina hatia ya kutenda mabaya wala ya kuasi. Wewe sijakukosea, lakini wewe unaniwinda mimi ili kuuondoa uhai wangu.
12 to judge LORD between me and between you and to avenge me LORD from you and hand my not to be in/on/with you
Bwana na ahukumu kati yangu na wewe. Naye Bwana alipize mabaya unayonitendea, lakini mkono wangu hautakugusa.
13 like/as as which to say proverb [the] eastern: older from wicked to come out: come wickedness and hand my not to be in/on/with you
Kama msemo wa kale usemavyo, ‘Kutoka kwa watenda maovu hutoka matendo maovu,’ kwa hiyo mkono wangu hautakugusa wewe.
14 after who? to come out: come king Israel after who? you(m. s.) to pursue after dog to die after flea one
“Je, mfalme wa Israeli ametoka dhidi ya nani? Ni nani unayemfuatia? Je, ni mbwa mfu? Ni kiroboto?
15 and to be LORD to/for judge and to judge between me and between you and to see: see and to contend [obj] strife my and to judge me from hand: power your
Bwana na awe mwamuzi wetu, yeye na aamue kati yetu. Yeye na anitetee shauri langu; anihesabie haki kwa kuniokoa mkononi mwako.”
16 and to be like/as to end: finish David to/for to speak: speak [obj] [the] word [the] these to(wards) Saul and to say Saul voice your this son: child my David and to lift: loud Saul voice his and to weep
Daudi alipomaliza kusema haya, Sauli akamuuliza, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Ndipo Sauli akalia kwa sauti kuu, akisema,
17 and to say to(wards) David righteous you(m. s.) from me for you(m. s.) to wean me [the] welfare and I to wean you [the] distress: evil
“Wewe ni mwenye haki kuliko mimi; umenitendea mema, lakini mimi nimekutendea mabaya.
18 (and you(m. s.) *Q(K)*) to tell [the] day: today [obj] which to make: do with me welfare [obj] which to shut me LORD in/on/with hand your and not to kill me
Sasa umeniambia juu ya mema uliyonitendea. Bwana alinitia mikononi mwako, lakini wewe hukuniua.
19 and for to find man: anyone [obj] enemy his and to send: let go him in/on/with way: journey pleasant and LORD to complete you welfare underneath: because of [the] day: today [the] this which to make: do to/for me
Je, mtu ampatapo adui yake, humwacha aende zake bila kumdhuru? Bwana na akulipe mema kwa jinsi ulivyonitenda leo.
20 and now behold to know for to reign to reign and to arise: establish in/on/with hand: power your kingdom Israel
Ninajua kwamba hakika utakuwa mfalme na ya kwamba ufalme wa Israeli utakuwa imara mikononi mwako.
21 and now to swear [emph?] to/for me in/on/with LORD if: surely no to cut: eliminate [obj] seed: children my after me and if: surely no to destroy [obj] name my from house: household father my
Sasa niapie kwa Bwana kwamba hutakatilia mbali uzao wangu wala kulifuta jina langu kutoka jamaa ya baba yangu.”
22 and to swear David to/for Saul and to go: went Saul to(wards) house: home his and David and human his to ascend: rise upon [the] fortress
Basi Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akarudi zake nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.