< 1 Samuel 23 >

1 and to tell to/for David to/for to say behold Philistine to fight in/on/with Keilah and they(masc.) to plunder [obj] [the] threshing floor
Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
2 and to ask David in/on/with LORD to/for to say to go: went and to smite in/on/with Philistine [the] these and to say LORD to(wards) David to go: went and to smite in/on/with Philistine and to save [obj] Keilah
Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
3 and to say human David to(wards) him behold we here in/on/with Judah afraid and also for to go: went Keilah to(wards) rank Philistine
Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
4 and to add: again still David to/for to ask in/on/with LORD and to answer him LORD and to say to arise: rise to go down Keilah for I to give: give [obj] Philistine in/on/with hand: power your
Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
5 and to go: went David (and human his *Q(K)*) Keilah and to fight in/on/with Philistine and to lead [obj] livestock their and to smite in/on/with them wound great: large and to save David [obj] to dwell Keilah
Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
6 and to be in/on/with to flee Abiathar son: child Ahimelech to(wards) David Keilah ephod to go down in/on/with hand: power his
Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
7 and to tell to/for Saul for to come (in): come David Keilah and to say Saul to alienate [obj] him God in/on/with hand: power my for to shut to/for to come (in): come in/on/with city door and bar
Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
8 and to hear: proclaim Saul [obj] all [the] people to/for battle to/for to go down Keilah to/for to confine to(wards) David and to(wards) human his
Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
9 and to know David for upon him Saul to plow/plot [the] distress: harm and to say to(wards) Abiathar [the] priest to approach: bring [emph?] [the] ephod
Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
10 and to say David LORD God Israel to hear: hear to hear: hear servant/slave your for to seek Saul to/for to come (in): come to(wards) Keilah to/for to ruin to/for city in/on/with for the sake of me
Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
11 to shut me master: men Keilah in/on/with hand: power his to go down Saul like/as as which to hear: hear servant/slave your LORD God Israel to tell please to/for servant/slave your and to say LORD to go down
Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
12 and to say David to shut master: men Keilah [obj] me and [obj] human my in/on/with hand: power Saul and to say LORD to shut
Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
13 and to arise: rise David and human his like/as six hundred man and to come out: come from Keilah and to go: went in/on/with in which to go: went and to/for Saul to tell for to escape David from Keilah and to cease to/for to come out: come
Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
14 and to dwell David in/on/with wilderness in/on/with stronghold and to dwell in/on/with mountain: hill country in/on/with wilderness Ziph and to seek him Saul all [the] day and not to give: give him God in/on/with hand: power his
Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
15 and to see: see David for to come out: come Saul to/for to seek [obj] soul: life his and David in/on/with wilderness Ziph in/on/with Horesh
Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
16 and to arise: rise Jonathan son: child Saul and to go: went to(wards) David Horesh and to strengthen: strengthen [obj] hand: power his in/on/with God
Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
17 and to say to(wards) him not to fear for not to find you hand: themselves Saul father my and you(m. s.) to reign upon Israel and I to be to/for you to/for second and also Saul father my to know so
Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
18 and to cut: make(covenant) two their covenant to/for face: before LORD and to dwell David in/on/with Horesh and Jonathan to go: went to/for house: home his
Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
19 and to ascend: rise Ziphite to(wards) Saul [the] Gibeah [to] to/for to say not David to hide with us in/on/with stronghold in/on/with Horesh in/on/with hill [the] Hachilah which from right: south [the] Jeshimon
Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
20 and now to/for all desire soul your [the] king to/for to go down to go down and to/for us to shut him in/on/with hand: power [the] king
Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
21 and to say Saul to bless you(m. p.) to/for LORD for to spare upon me
Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
22 to go: went please to establish: right still and to know and to see: see [obj] place his which to be foot his who? to see: see him there for to say to(wards) me be shrewd be shrewd he/she/it
Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
23 and to see: behold! and to know from all [the] refuge which to hide there and to return: return to(wards) me to(wards) to establish: establish and to go: went with you and to be if there he in/on/with land: country/planet and to search [obj] him in/on/with all thousand: clan Judah
Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
24 and to arise: rise and to go: went Ziph [to] to/for face: before Saul and David and human his in/on/with wilderness Maon in/on/with Arabah to(wards) right: south [the] Jeshimon
Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
25 and to go: went Saul and human his to/for to seek and to tell to/for David and to go down [the] crag and to dwell in/on/with wilderness Maon and to hear: hear Saul and to pursue after David wilderness Maon
Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
26 and to go: went Saul from side [the] mountain: mount from this and David and human his from side [the] mountain: mount from this and to be David to hurry to/for to go: went from face: before Saul and Saul and human his to surround to(wards) David and to(wards) human his to/for to capture them
Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
27 and messenger to come (in): come to(wards) Saul to/for to say to hasten [emph?] and to go: come [emph?] for to strip Philistine upon [the] land: country/planet
mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
28 and to return: return Saul from to pursue after David and to go: went to/for to encounter: toward Philistine upon so to call: call by to/for place [the] he/she/it Rock of Escape Rock of Escape
Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
29 and to ascend: rise David from there and to dwell in/on/with stronghold Engedi Engedi
Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.

< 1 Samuel 23 >