< 1 Kings 12 >

1 and to go: went Rehoboam Shechem for Shechem to come (in): come all Israel to/for to reign [obj] him
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 and to be like/as to hear: hear Jeroboam son: child Nebat and he/she/it still he in/on/with Egypt which to flee from face: because [the] king Solomon and to dwell Jeroboam in/on/with Egypt
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 and to send: depart and to call: call to to/for him (and to come (in): come *Q(K)*) Jeroboam and all assembly Israel and to speak: speak to(wards) Rehoboam to/for to say
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 father your to harden [obj] yoke our and you(m. s.) now to lighten from service father your [the] severe and from yoke his [the] heavy which to give: put upon us and to serve you
“Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 and to say to(wards) them to go: went still three day and to return: again to(wards) me and to go: went [the] people
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 and to advise [the] king Rehoboam with [the] old which to be to stand: stand with face: before Solomon father his in/on/with to be he alive to/for to say how? you(m. p.) to advise to/for to return: reply [obj] [the] people [the] this word
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 (and to speak: speak *Q(K)*) to(wards) him to/for to say if [the] day to be servant/slave to/for people [the] this and to serve them and to answer them and to speak: speak to(wards) them word pleasant and to be to/for you servant/slave all [the] day: always
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 and to leave: forsake [obj] counsel [the] old which to advise him and to advise with [the] youth which to magnify with him which [the] to stand: stand to/for face: before his
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 and to say to(wards) them what? you(m. p.) to advise and to return: reply word [obj] [the] people [the] this which to speak: speak to(wards) me to/for to say to lighten from [the] yoke which to give: put father your upon us
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 and to speak: speak to(wards) him [the] youth which to magnify with him to/for to say thus to say to/for people [the] this which to speak: speak to(wards) you to/for to say father your to honor: heavy [obj] yoke our and you(m. s.) to lighten from upon us thus to speak: speak to(wards) them little finger my to thicken from loin father my
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 and now father my to lift upon you yoke heavy and I to add upon yoke your father my to discipline [obj] you in/on/with whip and I to discipline [obj] you in/on/with scorpion
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 (and to come (in): come *Q(k)*) Jeroboam and all [the] people to(wards) Rehoboam in/on/with day [the] third like/as as which to speak: speak [the] king to/for to say to return: again to(wards) me in/on/with day [the] third
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 and to answer [the] king [obj] [the] people severe and to leave: forsake [obj] counsel [the] old which to advise him
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 and to speak: speak to(wards) them like/as counsel [the] youth to/for to say father my to honor: heavy [obj] yoke your and I to add upon yoke your father my to discipline [obj] you in/on/with whip and I to discipline [obj] you in/on/with scorpion
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 and not to hear: hear [the] king to(wards) [the] people for to be turn from from with LORD because to arise: establish [obj] word his which to speak: speak LORD in/on/with hand: by Ahijah [the] Shilonite to(wards) Jeroboam son: child Nebat
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 and to see: see all Israel for not to hear: hear [the] king to(wards) them and to return: reply [the] people [obj] [the] king word to/for to say what? to/for us portion in/on/with David and not inheritance in/on/with son: child Jesse to/for tent your Israel now to see: see house: household your David and to go: went Israel to/for tent his
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 and son: descendant/people Israel [the] to dwell in/on/with city Judah and to reign upon them Rehoboam
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 and to send: depart [the] king Rehoboam [obj] Adoram which upon [the] taskworker and to stone all Israel in/on/with him stone and to die and [the] king Rehoboam to strengthen to/for to ascend: copulate in/on/with chariot to/for to flee Jerusalem
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 and to transgress Israel in/on/with house: household David till [the] day: today [the] this
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
20 and to be like/as to hear: hear all Israel for to return: return Jeroboam and to send: depart and to call: call to [obj] him to(wards) [the] congregation and to reign [obj] him upon all Israel not to be after house: household David exception tribe Judah to/for alone him
Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
21 (and to come (in): come *Q(K)*) Rehoboam Jerusalem and to gather [obj] all house: household Judah and [obj] tribe Benjamin hundred and eighty thousand to choose to make: [do] battle to/for to fight with house: household Israel to/for to return: rescue [obj] [the] kingship to/for Rehoboam son: child Solomon
Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
22 and to be word [the] God to(wards) Shemaiah man [the] God to/for to say
Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
23 to say to(wards) Rehoboam son: child Solomon king Judah and to(wards) all house: household Judah and Benjamin and remainder [the] people to/for to say
“Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
24 thus to say LORD not to ascend: rise and not to fight [emph?] with brother: male-relative your son: descendant/people Israel to return: return man: anyone to/for house: home his for from with me to be [the] word: thing [the] this and to hear: hear [obj] word LORD and to return: again to/for to go: went like/as word LORD
‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
25 and to build Jeroboam [obj] Shechem in/on/with mountain: hill country Ephraim and to dwell in/on/with her and to come out: come from there and to build [obj] Peniel
Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
26 and to say Jeroboam in/on/with heart his now to return: return [the] kingdom to/for house: household David
Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
27 if to ascend: rise [the] people [the] this to/for to make: offer sacrifice in/on/with house: temple LORD in/on/with Jerusalem and to return: again heart [the] people [the] this to(wards) lord their to(wards) Rehoboam king Judah and to kill me and to return: return to(wards) Rehoboam king Judah
Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
28 and to advise [the] king and to make two calf gold and to say to(wards) them many to/for you from to ascend: rise Jerusalem behold God your Israel which to ascend: establish you from land: country/planet Egypt
Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
29 and to set: make [obj] [the] one in/on/with Bethel Bethel and [obj] [the] one to give: put in/on/with Dan
Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
30 and to be [the] word: thing [the] this to/for sin and to go: went [the] people to/for face: before [the] one till Dan
Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
31 and to make [obj] house: home high place and to make: do priest from end [the] people which not to be from son: descendant/people Levi
Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
32 and to make Jeroboam feast in/on/with month [the] eighth in/on/with five ten day to/for month like/as feast which in/on/with Judah and to ascend: offer up upon [the] altar so to make: do in/on/with Bethel Bethel to/for to sacrifice to/for calf which to make and to stand: put in/on/with Bethel Bethel [obj] priest [the] high place which to make
Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
33 and to ascend: rise upon [the] altar which to make in/on/with Bethel Bethel in/on/with five ten day in/on/with month [the] eighth in/on/with month which to devise (from heart his *Q(K)*) and to make: do feast to/for son: descendant/people Israel and to ascend: rise upon [the] altar to/for to offer: offer
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.

< 1 Kings 12 >