< 1 Chronicles 12 >
1 and these [the] to come (in): come to(wards) David to/for Ziklag still to restrain from face: before Saul son: child Kish and they(masc.) in/on/with mighty man to help [the] battle
Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
2 to handle bow to go right and to go left in/on/with stone and in/on/with arrow in/on/with bow from brother: male-relative Saul from Benjamin
walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
3 [the] head: leader Ahiezer and Joash son: child [the] Shemaah [the] Gibeathite (and Jeziel *Q(K)*) and Pelet son: child Azmaveth and Beracah and Jehu [the] Anathoth
Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
4 and Ishmaiah [the] Gibeonite mighty man in/on/with thirty and upon [the] thirty and Jeremiah and Jahaziel and Johanan and Jozabad [the] Gederathite
na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
5 Eluzai and Jerimoth and Bealiah and Shemariah and Shephatiah ([the] Haruphite *Q(K)*)
Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
6 Elkanah and Isshiah and Azarel and Joezer and Jashobeam [the] Korahite
Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
7 and Joelah and Zebadiah son: child Jeroham from [the] Gedor
Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
8 and from [the] Gad to separate to(wards) David to/for stronghold wilderness [to] mighty man [the] strength human army: war to/for battle to arrange shield and spear and face lion face their and like/as gazelle upon [the] mountain: mount to/for to hasten
Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
9 Ezer [the] head: leader Obadiah [the] second Eliab [the] third
Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
10 Mishmannah [the] fourth Jeremiah [the] fifth
Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
11 Attai [the] sixth Eliel [the] seventh
Atai wa sita, Elieli wa saba,
12 Johanan [the] eighth Elzabad [the] ninth
Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
13 Jeremiah [the] tenth Machbannai eleven ten
Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
14 these from son: descendant/people Gad head: leader [the] army one to/for hundred [the] small and [the] great: large to/for thousand
Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
15 these they(masc.) which to pass [obj] [the] Jordan in/on/with month [the] first and he/she/it to fill upon all (bank his *Q(K)*) and to flee [obj] all [the] valley to/for east and to/for west
Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
16 and to come (in): come from son: descendant/people Benjamin and Judah till to/for stronghold to/for David
Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
17 and to come out: come David to/for face: before their and to answer and to say to/for them if to/for peace: friendship to come (in): come to(wards) me to/for to help me to be to/for me upon you heart to/for unitedness and if to/for to deceive me to/for enemy my in/on/with not violence in/on/with palm my to see: see God father our and to rebuke
Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
18 and spirit to clothe [obj] Amasai head: leader ([the] officer *Q(K)*) to/for you David and with you son: child Jesse peace peace to/for you and peace to/for to help you for to help you God your and to receive them David and to give: put them in/on/with head: leader [the] band
Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
19 and from Manasseh to fall: deserting upon David in/on/with to come (in): come he with Philistine upon Saul to/for battle and not to help them for in/on/with counsel to send: depart him lord Philistine to/for to say in/on/with head our to fall: deserting to(wards) lord his Saul
Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
20 in/on/with to go: went he to(wards) Ziklag to fall: deserting upon him from Manasseh Adnah and Jozabad and Jediael and Michael and Jozabad and Elihu and Zillethai head: leader [the] thousand which to/for Manasseh
Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
21 and they(masc.) to help with David upon [the] band for mighty man strength all their and to be ruler in/on/with army
Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
22 for to/for time day: daily in/on/with day: daily to come (in): come upon David to/for to help him till to/for camp great: large like/as camp God
Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
23 and these number head: group [the] to arm to/for army to come (in): come upon David Hebron [to] to/for to turn: turn royalty Saul to(wards) him like/as lip: word LORD
Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
24 son: descendant/people Judah to lift: bear shield and spear six thousand and eight hundred to arm army
watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
25 from son: descendant/people Simeon mighty man strength to/for army: war seven thousand and hundred
Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
26 from son: descendant/people [the] Levi four thousand and six hundred
Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
27 and Jehoiada [the] leader to/for Aaron and with him three thousand and seven hundred
pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
28 and Zadok youth mighty man strength and house: household father his ruler twenty and two
na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
29 and from son: descendant/people Benjamin brother: male-relative Saul three thousand and till here/thus greatness their to keep: obey charge house: household Saul
Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
30 and from son: descendant/people Ephraim twenty thousand and eight hundred mighty man strength human name to/for house: household father their
Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
31 and from half tribe Manasseh eight ten thousand which to pierce in/on/with name to/for to come (in): come to/for to reign [obj] David
Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
32 and from son: descendant/people Issachar to know understanding to/for time to/for to know what? to make: do Israel head: leader their hundred and all brother: male-relative their upon lip: word their
Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
33 from Zebulun to come out: regular army: war to arrange battle in/on/with all article/utensil battle fifty thousand and to/for to help in/on/with not heart and heart
Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
34 and from Naphtali ruler thousand and with them in/on/with shield and spear thirty and seven thousand
Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
35 and from [the] Danite to arrange battle twenty and eight thousand and six hundred
Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
36 and from Asher to come out: regular army: war to/for to arrange battle forty thousand
Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
37 and from side: beyond to/for Jordan from [the] Reubenite and [the] Gad and half tribe: staff Manasseh in/on/with all article/utensil army: war battle hundred and twenty thousand
Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
38 all these human battle to help rank in/on/with heart complete to come (in): come Hebron [to] to/for to reign [obj] David upon all Israel and also all remnant Israel heart one to/for to reign [obj] David
Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
39 and to be there with David day three to eat and to drink for to establish: prepare to/for them brother: male-sibling their
Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
40 and also [the] near to(wards) them till Issachar and Zebulun and Naphtali to come (in): come food in/on/with donkey and in/on/with camel and in/on/with mule and in/on/with cattle food flour fig cake and cluster and wine and oil and cattle and flock to/for abundance for joy in/on/with Israel
Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.