< 1 Chronicles 10 >

1 and Philistine to fight in/on/with Israel and to flee man Israel from face: before Philistine and to fall: kill slain: killed in/on/with mountain: mount (Mount) Gilboa
Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika mlima Gilboa.
2 and to cleave Philistine after Saul and after son: child his and to smite Philistine [obj] Jonathan and [obj] Abinadab and [obj] Malchi-shua Malchi-shua son: child Saul
Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
3 and to honor: heavy [the] battle upon Saul and to find him [the] to shoot in/on/with bow and to twist: writh in pain from [the] to shoot
Mapigano yakawa makali kumzunguka Sauli na wakati wapiga mishale walipompata, wakamjeruhi.
4 and to say Saul to(wards) to lift: bearing(armour) article/utensil his to draw sword your and to pierce me in/on/with her lest to come (in): come [the] uncircumcised [the] these and to abuse in/on/with me and not be willing to lift: bearing(armour) article/utensil his for to fear much and to take: take Saul [obj] [the] sword and to fall: fall upon her
Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 and to see: see to lift: bearing(armour) article/utensil his for to die Saul and to fall: fall also he/she/it upon [the] sword and to die
Mbeba silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, naye pia akauangukia upanga wake akafa.
6 and to die Saul and three son: child his and all house: household his together to die
Kwa hiyo Sauli na wanawe watatu wakafa, pamoja na nyumba yake yote.
7 and to see: see all man Israel which in/on/with valley for to flee and for to die Saul and son: child his and to leave: forsake city their and to flee and to come (in): come Philistine and to dwell in/on/with them
Waisraeli wote waliokuwa bondeni walipoona kwamba jeshi limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliacha miji yao wakakimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 and to be from morrow and to come (in): come Philistine to/for to strip [obj] [the] slain: killed and to find [obj] Saul and [obj] son: child his to fall: fall in/on/with mountain: mount (Mount) Gilboa
Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe wameanguka katika Mlima Gilboa.
9 and to strip him and to lift: raise [obj] head his and [obj] article/utensil his and to send: depart in/on/with land: country/planet Philistine around: whole to/for to bear tidings [obj] idol their and [obj] [the] people
Wakamvua mavazi, wakachukua kichwa chake pamoja na silaha zake, wakawatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari hizi miongoni mwa sanamu zao na watu wao.
10 and to set: put [obj] article/utensil his house: temple God their and [obj] head his to blow house: temple Dagon
Waliweka silaha zake katika hekalu la miungu yao, wakatundika kichwa chake katika hekalu la Dagoni.
11 and to hear: hear all Jabesh (Jabesh)-gilead [obj] all which to make: do Philistine to/for Saul
Wakazi wote wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yote Wafilisti waliyomtendea Sauli,
12 and to arise: rise all man strength and to lift: bear [obj] body Saul and [obj] body son: child his and to come (in): bring them Jabesh (Gilead) [to] and to bury [obj] bone their underneath: under [the] oak in/on/with Jabesh (Gilead) and to fast seven day
mashujaa wao wote wakaondoka, wakautwaa mwili wa Sauli na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi. Wakaizika mifupa yao chini ya mti mkubwa huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.
13 and to die Saul in/on/with unfaithfulness his which be unfaithful in/on/with LORD upon word LORD which not to keep: obey and also to/for to ask in/on/with medium to/for to seek
Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Bwana. Hakulishika neno la Bwana, hata akataka shauri kwa mwaguzi kwa ajili ya uongozi,
14 and not to seek in/on/with LORD and to die him and to turn: turn [obj] [the] kingship to/for David son: child Jesse
hakumuuliza Bwana. Kwa hiyo Bwana alimuua, na ufalme akampa Daudi mwana wa Yese.

< 1 Chronicles 10 >