< Zephaniah 2 >

1 Gather yourselves together and gather together O nation not ashamed.
Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
2 Before brings forth a decree like chaff it has passed away a day before - not it will come on you [the] burning of [the] anger of Yahweh before not it will come on you [the] day of [the] anger of Yahweh.
kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
3 Seek Yahweh O all [the] humble [people] of the land who judgment his they have done seek righteousness seek humility perhaps you will be hidden on [the] day of [the] anger of Yahweh.
Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
4 For Gaza abandoned it will be and Ashkelon [will become] a desolation Ashdod at the noontide people will drive out it and Ekron it will be plucked up.
Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
5 Woe to! [the] inhabitants of [the] region of the sea [the] nation of [the] Kerethites [the] word of Yahweh [is] on you O Canaan [the] land of [the] Philistines and I will destroy you from not inhabitant.
Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
6 And it will be [the] region of the sea pastures of meadows of shepherds and folds of sheep.
Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
7 And it will belong [the] region to [the] remnant of [the] house of Judah on them they will graze! in [the] houses of Ashkelon in the evening they will lie down! for he will visit them Yahweh God their and he will turn back (captivity their. *Q(k)*)
Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
8 I have heard [the] reproach of Moab and [the] reviling words of [the] people of Ammon who they have reproached people my and they have magnified themselves on territory their.
“Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
9 Therefore [by] [the] life of me [the] utterance of Yahweh of hosts [the] God of Israel that Moab like Sodom it will be and [the] people of Ammon like Gomorrah a place possessed of nettle[s] and a pit of salt and a waste until perpetuity [the] remnant of people my they will plunder them and [the] rest ofK: (nation my *Q(K)*) they will take possession of them.
Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
10 This [will belong] to them in place of pride their for they reproached and they magnified themselves on [the] people of Yahweh of hosts.
Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
11 [will be] awesome Yahweh on them if he will make lean all [the] gods of the earth so they may bow down to him everyone from own place his all [the] islands of the nations.
Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
12 Also you O Cushites [are those] slain of sword my they.
“Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
13 And he may stretch out hand his on [the] north so he may destroy Assyria and he may make Nineveh a waste a dry region like the wilderness.
Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
14 And they will lie down in [the] midst of it herds every animal of a nation both desert owl as well as hedgehog on capitals its they will spend [the] night a sound it will sing in the window desolation [will be] on the threshold for cedar-work he will lay bare.
Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
15 This [is] the city jubilant which dwells to security which says in heart its I and only I [am] yet how! - it has become a waste a resting place for animal[s] every [one who] passes by at it he will hiss he will shake hand his.
Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.

< Zephaniah 2 >