< Revelation 13 >
1 And (he stood *N(K)O*) upon the sand of the sea. And I saw out of the sea a beast rising, having horns ten and heads seven and on the horns of it ten royal crowns and upon the heads of it (names *N(K)O*) of blasphemy.
Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
2 And the beast that I saw was like as a leopard and the feet of it like (a bear’s *N(k)O*) and the mouth of it like [the] mouth of a lion. And gave to it the dragon the power of him and the throne of him and authority great.
Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
3 And (I saw *K*) one of the heads of it ([was] as *NK(o)*) slain to death, And the wound the of death of it was healed, and (marveled *NK(o)*) (in *ko*) all ([on] the earth *NK(o)*) after the beast.
Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
4 And they worshiped (the dragon *N(k)O*) (that *N(k)(o)*) (gave *NK(o)*) authority to the beast and they worshiped (the beast *N(k)O*) saying; Who [is] like as the beast (And *no*) who (is able *NK(o)*) to make war against it?
Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
5 And was given to it a mouth speaking great things and (blasphemies *NK(o)*) and was given to it authority (war *O*) to act months forty (and *no*) two.
Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
6 And it opened the mouth of it unto (blasphemies *N(k)O*) against God to blaspheme the name of Him and the tabernacle of Him, (and *k*) those in heaven dwelling.
Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
7 And there was given to it to make war with the saints and to overcome them And was given to it authority over every tribe (and people *NO*) and tongue and nation.
Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
8 And will worship (it *N(k)O*) all those dwelling on the earth, (each of whom *N(k)O*) not have been written (the name *N(k)O*) (of him *no*) in (the book *N(k)O*) of life of the Lamb which slain from [the] founding of [the] world.
Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
9 If anyone has an ear, he should hear.
Yeye aliye na sikio na asikie.
10 If anyone (into *n(o)*) captivity (gathers *K*) into captivity he goes, If anyone with [the] sword (is to be killed, *N(k)O*) (it is necessary for *ko*) him by [the] sword [is] to be killed; Here is the endurance and the faith of the saints.
Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
11 And I saw another beast rising out of the earth, and it had horns two like as a lamb and it was speaking like a dragon.
Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
12 And the authority of the first beast all it exercises on behalf of it and (makes *NK(o)*) the earth and those in it dwelling that (they will worship *N(k)O*) the beast first, of whom was healed the wound the fatal of it.
Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
13 And it works signs great so that even fire it may cause out of heaven (to come down to *NK(o)*) the earth in the presence of men.
Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
14 And it deceives (those *k*) (mine *O*) who dwelling on the earth through the signs that were given to it to perform before the beast telling to those dwelling on the earth to make an image to the beast (that *N(k)O*) (has *NK(o)*) the wound (from *o*) of the sword and has lived.
Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
15 And there was given (to it *NK(o)*) to give breath to the image of the beast so that also may speak the image of the beast, and may cause that as many as (might *N(k)O*) not shall worship (the image *N(k)O*) of the beast shall be killed.
Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
16 And it causes all the small and the great and the rich and the poor and the free and the servants, that (it may give *N(k)(o)*) to them (a mark *N(k)O*) on the hand of them right or on (the *N(k)O*) (forehead *N(K)O*) of them,
Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
17 and that no one (may be able *NK(o)*) to buy or to sell only except the [one] having the mark — (or *K*) the name of the beast or the number of the name of it.
ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
18 Here the wisdom is. The [one] having (*k*) understanding he should count the number of the beast, number for a man’s it is, and the number of it (is *o*) (six hundred sixty *N(K)O*) (six. *N(k)O*)
Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.