< Psalms 75 >

1 To the choirmaster al-tashcheth a psalm of Asaph a song. We give thanks to you - O God we give thanks and [is] near name your people recount wonders your.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 If I will take an appointed time I uprightness I will judge.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 [are] melting away [the] earth And all inhabitants its I I put in order pillars its (Selah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 I say to the boasters may not you boast and to the wicked [people] may not you lift up a horn.
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 May not you lift up to the height horn your may you speak with a neck arrogance.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 For not [is] from [the] going out and from [the] setting place and not from [the] wilderness exaltation.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 For God [is the] judge this one he brings low and this one he lifts up.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 For a cup [is] in [the] hand of Yahweh and wine it is foaming - full spiced drink and he has poured out some of this surely dregs its they will drain they will drink all [the] wicked [people] of [the] earth.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 And I I will declare for ever I will sing praises to [the] God of Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 And all [the] horns of wicked [people] I will cut off they will be lifted up [the] horns of [the] righteous.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psalms 75 >