< Psalms 73 >

1 A psalm of Asaph surely [is] good to Israel God to [people] pure of heart.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 And I like a little (they had turned aside *Q(K)*) feet my like nothing (they had been poured out *Q(K)*) steps my.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 For I was jealous of the boasters [the] well-being of wicked [people] I saw.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 That there not [are] pangs to death their and [is] fat body their.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 [are] in [the] trouble of Humankind not they and with humankind not they are stricken.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Therefore [it is] a necklace [for] them pride it covers a garment of violence them.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 It comes out from fat eye their they pass over [the] imaginations of heart.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 They mock - and they may speak with evil oppression from a high place they speak.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 They set in the heavens mouth their and tongue their it walks on the earth.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Therefore - (it turns back *Q(K)*) people his here and waters of full they are drained by them.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 And they say how? does he know God and [is] there? knowledge with [the] Most High.
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Here! these [are] wicked [people] and [people] at ease of perpetuity they increase wealth.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Surely vanity I have kept pure heart my and I have washed in innocence hands my.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 And I have been stricken all the day and rebuke my [has been] to the mornings.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 If I had said I will speak like here! [the] generation of children your I dealt treacherously with.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 And I thought! to know this [was] trouble (it *Q(K)*) in view my.
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Until I went into [the] sanctuari of God I considered end their.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Surely on slippery [places] you set them you make fall them to deceptions.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 How! they have become a waste like a moment they come to an end they are finished from sudden terror.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Like a dream from when awakes O Lord when waken - image their you will despise.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 If it was embittered heart my and kidneys my I was pierced.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 And I [was] stupid and not I knew animals I was with you.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 And I continually [am] with you you take hold on [the] hand of right my.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 With counsel your you guide me and after honor you will take me.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Who? [belongs] to me in the heavens and with you not I take pleasure on the earth.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 It had come to an end flesh my and heart my [is] [the] rock of heart my and portion my God for ever.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 For there! [people] far from you they will perish you destroy every [one who] acts as a prostitute from you.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 And I - [the] approach of God for me [is] good I have made - in [the] Lord Yahweh refuge my to recount all works your.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalms 73 >