< Psalms 50 >

1 A psalm of Asaph God - God Yahweh he has spoken and he has summoned [the] earth from [the] rising of [the] sun to setting its.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 From Zion perfection of beauty God he has shone forth.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 He comes God our and may not he be silent fire before him it consumes and around him it is tempestuous exceedingly.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He summons the heavens above and the earth to judge people his.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Gather to me O faithful [people] my [those who] made covenant my with sacrifice.
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 And they declared [the] heavens righteousness his for God - [is] judge he (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Hear! O people my - so let me speak O Israel and I will warn you [am] God God your I.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Not on sacrifices your I rebuke you and burnt offerings your [are] to before me continually.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Not I will accept from household your a young bull from folds your goats.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 For [belong] to me every living creature of [the] forest [the] animals on hills of a thousand.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know every bird of [the] mountains and moving creature[s] of [the] field [are] with me.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 If I will be hungry not I will tell to you for [belong] to me [the] world and what fills it.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 ¿ Do I eat [the] flesh of mighty [bulls] and [the] blood of goats do I drink?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Sacrifice to God a thank-offering and pay to [the] Most High vows your.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 And call out to me in a day of trouble I will rescue you and you will honor me.
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 And to the wicked - he says God what? [is] to you to recount decrees my and you have taken covenant my on mouth your.
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 And you you hate discipline and you have thrown words my behind you.
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 If you saw a thief and you were pleased with him and [was] with adulterers portion your.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Mouth your you let loose in evil and tongue your it harnesses deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 You sit on brother your you speak on [the] child of mother your you give a fault.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 These [things] you have done - and I kept silent you imagined exactly I am like you I will rebuke you and I will arrange to eyes your.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Consider please this O [those who] forget God lest I should tear to pieces and there not [will be] a deliverer.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 [one who] sacrifices A thank-offering he honors me and [one who] sets a way I will let look him on [the] salvation of God.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >