< Psalms 48 >

1 A song a psalm of [the] sons of Korah. [is] great Yahweh and [is] to be praised exceedingly in [the] city of God our [the] mountain of holiness his.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 [it is] beautiful of Height [the] joy of all the earth [the] mountain of Zion [the] remotest parts of Zaphon [the] town of [the] king great.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God [is] in fortresses its he has made himself known to a refuge.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For there! the kings they assembled they passed on together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 They they saw thus they were astonished they were terrified they hurried away.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling it seized them there anguish like [woman] giving birth.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 With a wind of [the] east you shatter ships of Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Just as we have heard - so we have seen in [the] city of Yahweh of hosts in [the] city of God our God he will establish it until perpetuity (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 We have reflected on O God covenant loyalty your in [the] midst of temple your.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Like name your O God so praise your [is] over [the] ends of [the] earth righteousness it is full right [hand] your.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 It will rejoice - [the] mountain of Zion they will be glad [the] daughters of Judah on account of judgments your.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Go around Zion and go round it count towers its.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Set heart your - to rampart its walk through fortresses its so that you may recount [it] to a generation later.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 For this - [is] God God our forever and ever he he will guide us on dying.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psalms 48 >