< Psalms 46 >
1 To the choirmaster of [the] sons of Korah on alamoth a song. God of us [is] a refuge and strength a help in troubles he is found exceedingly.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 There-fore not we will fear when changes [the] earth and when shake mountains in [the] heart of [the] seas.
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 They will roar they will foam waters its they will shake mountains at swelling its (Selah)
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 A river streams its they make glad [the] city of God [the] holy [place] of [the] dwellings of [the] Most High.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 God [is] in midst its not it will be shaken he will help it God to [the] turning of [the] morning.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 They were in a tumult nations they shook kingdoms he gave with voice his it melted [the] earth.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 Yahweh of hosts [is] with us [is] a refuge of us [the] God of Jacob (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Come see [the] works of Yahweh who he has appointed desolations on the earth.
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 [he is] making cease Wars to [the] end of the earth bow[s] he breaks and he cuts in two spear[s] carts he burns with fire.
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
10 Be quiet and know that I [am] God I will be exalted among the nations I will be exalted on the earth.
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
11 Yahweh of hosts [is] with us [is] a refuge of us [the] God of Jacob (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.