< Psalms 4 >

1 To the choirmaster with stringed instruments a psalm of David. When call I answer me - O God of righteousness my in the distress you have made wide for me show favor to me and hear prayer my.
Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
2 O sons of man until when? [will] honor my [become] ignominy will you love?! vanity will you seek? falsehood (Selah)
Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
3 And know that he has set apart Yahweh [the] faithful for himself Yahweh he will hear when call I to him.
Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
4 Tremble and may not you sin speak in heart your on bed your and be silent (Selah)
Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
5 Sacrifice sacrifices of righteousness and trust to Yahweh.
Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
6 Many [people] [are] saying who? will he show us good lift up! on us [the] light of face your O Yahweh.
Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
7 You have put joy in heart my more than a time [when] grain their and new wine their they abound.
Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
8 In peace together I will lie down and I may sleep for you O Yahweh alone to security you caused to dwell me.
Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.

< Psalms 4 >