< Psalms 30 >
1 A psalm [the] song of [the] dedication of the house of David. I will exalt you O Yahweh for you have drawn up me and not you have allowed to rejoice enemies my to me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 O Yahweh God my I cried for help to you and you healed me.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 O Yahweh you brought up from Sheol life my you preserved alive me (from going down my *Q(K)*) [the] pit. (Sheol )
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
4 Sing praises to Yahweh O faithful [people] his and give thanks to [the] remembrance of holiness his.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 For a moment - [is] in anger his life [is] in favor his in the evening it passes [the] night weeping and to the morning a shout of joy.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 And I I said in prosperity my not I will be shaken for ever.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 O Yahweh in favor your you made stand to mountain my strength you hid face your I was disturbed.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 To you O Yahweh I called out and to [the] Lord I sought favor.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 What? [is the] profit in blood my in going down my to [the] pit ¿ will it give thanks to you dust ¿ will it declare faithfulness your.
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Hear O Yahweh and show favor to me O Yahweh be a helper of me.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 You turned wailing my into dancing to me you loosened sackcloth my and you girded me joy.
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 So that - it may sing praises to you honor and not it may be silent O Yahweh God my for ever I will give thanks to you.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.