< Psalms 112 >

1 Praise Yahweh - how blessed! [is] a person fearing Yahweh in commandments his he delights exceedingly.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Mighty in the land it will be offspring his [the] generation of upright [people] it will be blessed.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Wealth and rich[es] [are] in house his and righteousness his [is] enduring for ever.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 It rises in the darkness light for the upright [people] [the] gracious and [the] compassionate and [the] righteous.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 [is] good A person [who] shows favor and [who] lends he maintains affairs his with justice.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 For for ever not he will be shaken a memory of perpetuity he will become a righteous [person].
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 From new[s] bad not he will be afraid [is] steadfast heart his trusting in Yahweh.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 [is] supported Heart his not he will be afraid until that he will look on foes his.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 He scatters - he gives to needy [people] righteousness his [is] enduring for ever horn his it will be exalted in honor.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 A wicked [person] he will see - and he will be angry teeth his he will gnash and he will melt away [the] desire of wicked [people] it will perish.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

< Psalms 112 >