< Psalms 106 >

1 Praise Yahweh - give thanks to Yahweh for [he is] good for [is] for ever covenant loyalty his.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Who? will he tell [the] mighty deeds of Yahweh will he proclaim? all praise his.
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 How blessed! [are those who] observe justice [one who] does righteousness at every time.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Remember me O Yahweh with [the] favor of people your visit me with salvation your.
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 To look - on [the] good thing[s] of chosen ones your to rejoice in [the] joy of nation your to boast with inheritance your.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 We have sinned with ancestors our we have done wrong we have acted wickedly.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Ancestors our in Egypt - not they considered wonders your not they remembered [the] greatness of covenant loyalti your and they rebelled at [the] sea at [the] sea of reed[s].
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 And he saved them for [the] sake of name his to make known might his.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 And he rebuked [the] sea of reed[s] and it dried up and he led them in the deeps like the wilderness.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 And he saved them from [the] hand of [one who] hated and he redeemed them from [the] hand of an enemy.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 And they covered [the] waters opponents their one from them not he was left.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 And they believed words his they sang praise his.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 They made haste they forgot works his not they waited for counsel his.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 And they craved a craving in the wilderness and they put to [the] test God in a desolate place.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 And he gave to them petition their and he sent a wasting disease on self their.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 And they were envious of Moses in the camp of Aaron [the] holy [one] of Yahweh.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 It opened [the] earth and it swallowed up Dathan and it covered over [the] company of Abiram.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 And it burned fire among company their flame it burned up [the] wicked [people].
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 They made a calf at Horeb and they bowed down to a molten image.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 And they exchanged glory their for an image of an ox [which] eats vegetation.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 They forgot God deliverer their [who] did great [things] in Egypt.
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Wonders in [the] land of Ham awesome [deeds] at [the] sea of reed[s].
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 And he said to destroy them if not Moses chosen one his he had stood in the breach before him to turn back anger his from destroying.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 And they rejected [the] land of desire not they believed word his.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 And they murmured in tents their not they listened to [the] voice of Yahweh.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 And he raised hand his to them to make fall them in the wilderness.
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 And to make fall offspring their among the nations and to scatter them among the lands.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 And they joined themselves to Baal Peor and they ate sacrifices of dead [ones].
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 And they provoked to anger by deeds their and it broke out among them a plague.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 And he stood up Phinehas and he mediated and it was restrained the plague.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 And it was reckoned to him to righteousness to a generation and a generation until perpetuity.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 And they provoked to anger at [the] waters of Meribah and it was bad for Moses because of them.
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 For they rebelled toward spirit his and he spoke rashly with lips his.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Not they destroyed the peoples which he had said Yahweh to them.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 And they mixed themselves with the nations and they learned deeds their.
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 And they served idols their and they became for them a snare.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 And they sacrificed sons their and daughters their to demons.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 And they shed blood innocent [the] blood of sons their and daughters their whom they sacrificed to [the] idols of Canaan and it was polluted the land by the blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 And they became unclean by works their and they played [the] prostitute by deeds their.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 And it burned [the] anger of Yahweh on people his and he abhorred inheritance his.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 And he gave them in [the] hand of nations and they ruled over them [those who] hated them.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 And they oppressed them enemies their and they were humbled under hand their.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Times many he delivered them and they they rebelled by plan[s] their and they sank by iniquity their.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 And he saw when it was distress to them when heard he cry of entreaty their.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 And he remembered to them covenant his and he relented according to [the] greatness of (covenant loyalti his. *Q(K)*)
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 And he made them into compassion before all captors their.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Save us - O Yahweh God our and gather us from the nations to give thanks to [the] name of holiness your to boast in praise your.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 [be] blessed Yahweh [the] God of Israel from antiquity - and until perpetuity and it will say all the people amen praise Yahweh.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psalms 106 >