< Proverbs 28 >

1 They flee and there not [is one who] pursues [the] wicked and righteous [people] like a young lion he is confident.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 By [the] transgression of a land [are] many princes its and by a person understanding knowing thus it will last long.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 A man poor and [who] oppresses poor [people] rain [which] washes away and there not [is] food.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 [those who] forsake [the] law They praise [the] wicked and [those who] keep [the] law they engage in strife with them.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 People of evil not they understand justice and [those who] seek Yahweh they understand everything.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 [is] good A poor [person] [who] walks in integrity his more than [the] [person] perverse of two ways and he [is] rich.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 [one who] keeps [the] law [is] a son Understanding and [one who] associates with gluttons he shames father his.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 [one who] increases Wealth his by interest (and usury *Q(K)*) for [one who] shows favor to poor [people] he gathers it.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 [one who] turns aside Ear his from hearing [the] law also prayer his [is] an abomination.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 [one who] leads astray Upright [people] - in a way evil in own pit his he he will fall and blameless [people] they will inherit good.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 [is] wise In own eyes his a person rich and a poor [person] understanding he examines thoroughly him.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 When rejoice righteous [people] great glory and when arise wicked [people] he is searched for everyone.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 [one who] conceals Transgressions his not he will prosper and [one who] confesses and [one who] forsakes [them] he will be shown mercy.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 How blessed! [is] a person [who] fears continually and [one who] hardens heart his he will fall in calamity.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 A lion roaring and a bear rushing a ruler wicked over a people poor.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 A ruler lacking of understanding and great of extortion ([one who] hates *Q(K)*) unjust gain he will prolong days.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 A person oppressed by [the] blood of a life to [the] pit he will flee may not people support him.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 [one who] walks Blameless he will be delivered and [one who] is crooked of two ways he will fall at one.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 [one who] tills Land his he will be satisfied food and [one who] pursues empty [things] he will be satisfied poverty.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 A person of faithfulness [will be] great of blessings and [one who] hastens to gain riches not he will go unpunished.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 To pay regard to face not [is] good and on a piece of bread he will transgress a man.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 [is] hastening To wealth a person evil of eye and not he knows that poverty it will come to him.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 [one who] reproves A person after me favor he will find more than [one who] makes smooth [the] tongue.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 [one who] robs - Father his and mother his and [one who] says there not [is] a transgression [is] a companion he of a person of destruction.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 A [person] arrogant of self he stirs up strife and [one who] relies on Yahweh he will be made fat.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 [one who] trusts In own heart his he [is] a fool and [one who] walks in wisdom he he will be delivered.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 [one who] gives To the poor there not [is] lack and [one who] hides eyes his great of curses.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 When arise wicked [people] he hides himself everyone and when perish they they increase righteous [people].
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.

< Proverbs 28 >