< Proverbs 23 >

1 If you will sit down to eat with a ruler carefully you will consider [that] which [is] before you.
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 And you will put a knife in throat your if [are] a master of appetite you.
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 May not (you crave *Q(K)*) for dainties his and it [is] food of lies.
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 May not you labor to gain riches from understanding your cease.
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 (¿ Do you cause to fly *Q(K)*) eyes your on it and there not [is] it for certainly it makes for itself wings like an eagle (it flies away *Q(K)*) the heavens.
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 May not you eat [the] food of a [person] evil of eye and may not (you crave *Q(K)*) for dainties his.
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 For - as he calculates in self his [is] so he eat and drink he says to you and heart his not [is] with you.
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 Morsel your [which] you have eaten you will vomit up it and you will spoil words your pleasant.
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 In [the] ears of a fool may not you speak for he will despise [the] insight of words your.
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 May not you displace a boundary of antiquity and in [the] fields of fatherless ones may not you go.
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 For redeemer their [is] strong he he will conduct case their with you.
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 Bring! to discipline heart your and ears your to words of knowledge.
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 May not you withhold from a youth discipline for you will strike him with the rod not he will die.
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 You with the rod you will strike him and life his from Sheol you will deliver. (Sheol h7585)
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
15 O son my if it is wise heart your it will rejoice heart my also I.
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 So they may rejoice kidneys my when speak lips your uprightness.
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 May not it be jealous heart of your sinners that except in [the] fear of Yahweh all the day.
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 That except there [is] a future and hope your not it will be cut off.
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Listen O you son my and be wise and guide in the way heart your.
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 May not you be among drunkards of wine among gluttons of meat themselves.
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 For a drunkard and a glutton he will become impoverished and rags it will clothe [them] drowsiness.
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Listen to father your who he begot you and may not you despise if she is old mother your.
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Truth buy and may not you sell [it] wisdom and discipline and understanding.
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 (Certainly he rejoices *Q(k)*) [the] father of a righteous [son] (and [one who] begets *Q(K)*) a wise [son] (he rejoices *Q(K)*) in him.
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 May he rejoice father your and mother your and may she rejoice [the] [one who] bore you.
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 Give! O son my heart your to me and eyes your ways my (let them observe. *Q(K)*)
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 For [is] a pit deep a prostitute and [is] a well narrow a foreign [woman].
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 Also she like a robber she lies in wait and treacherous [people] among humankind she increases.
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 [belongs] to Whom? woe [belongs] to whom? woe! [belong] to whom? (contentions *Q(K)*) [belongs] to whom? complaint [belong] to whom? wounds without cause [belongs] to whom? dullness of eyes.
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 To [those who] delay over the wine to [those who] go to examine mixed wine.
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 May not you see wine for it will be red if it will give (in the cup *Q(K)*) eye its it will go with smoothness.
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 End its like a snake it will bite and like a viper it will sting.
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 Eyes your they will see strange [things] and heart your it will speak perverse things.
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 And you will be like [one who] lies down in [the] heart of [the] sea and like [one who] lies down at [the] top of a mast.
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 They struck me not I am sick they beat me not I know when? will I awake I will repeat I will seek it again.
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”

< Proverbs 23 >