< Numbers 27 >

1 And they drew near [the] daughters of Zelophehad [the] son of Hepher [the] son of Gilead [the] son of Makir [the] son of Manasseh of [the] clans of Manasseh [the] son of Joseph and these [were] [the] names of daughters his Mahlah Noah and Hoglah and Milcah and Tirzah.
Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
2 And they took their stand before Moses and before Eleazar the priest and before the leaders and all the congregation [the] entrance of [the] tent of meeting saying.
ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
3 Father our he died in the wilderness and he not he was in among the company which gathered on Yahweh in [the] company of Korah for in own sin his he died and sons not they belonged to him.
“Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
4 Why? will it be withdrawn [the] name of father our from among clan his for not [belonged] to him a son give! to us a possession in among [the] brothers of father our.
Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
5 And he brought near Moses case their before Yahweh.
Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
6 And he said Yahweh to Moses saying.
naye Bwana akamwambia Mose,
7 Right [the] daughters of Zelophehad [are] speaking certainly you will give to them possession of an inheritance in among [the] brothers of father their and you will make pass over [the] inheritance of father their to them.
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8 And to [the] people of Israel you will speak saying a man if he will die and a son not [belongs] to him and you will make pass over inheritance his to daughter his.
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9 And if not [belongs] to him a daughter and you will give inheritance his to brothers his.
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10 And if not [belong] to him brothers and you will give inheritance his to [the] brothers of father his.
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
11 And if not brothers [belong] to father his and you will give inheritance his to relative his near to him from own clan his and he will take possession of it and it will become for [the] people of Israel a statute of judgment just as he has commanded Yahweh Moses.
Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
12 And he said Yahweh to Moses go up to [the] mountain of the Abarim this and see the land which I have given to [the] people of Israel.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
13 And you will see it and you will be gathered to people your also you just as he was gathered Aaron brother your.
Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
14 Since you rebelled against mouth my in [the] wilderness of Zin in [the] strife of the congregation to treat as holy me at the waters to eyes their they [were] [the] waters of Meribath Kadesh [the] wilderness of Zin.
kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
15 And he spoke Moses to Yahweh saying.
Mose akamwambia Bwana,
16 Let him appoint Yahweh [the] God of the spirits of all flesh a man over the congregation.
“Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
17 Who he will go out before them and who he will come before them and who he will lead out them and who he will bring them and not it will be [the] congregation of Yahweh like sheep which not [belongs] to them a shepherd.
ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
18 And he said Yahweh to Moses take for yourself Joshua [the] son of Nun a man whom a spirit [is] in him and you will lay hand your on him.
Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
19 And you will make stand him before Eleazar the priest and before all the congregation and you will commission him to eyes their.
Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
20 And you will put some of majesty your on him so that they may hear all [the] congregation of [the] people of Israel.
Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
21 And before Eleazar the priest he will stand and he will enquire for him by [the] judgment of the Urim before Yahweh on mouth his they will go out and on mouth his they will come he and all [the] people of Israel with him and all the congregation.
Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
22 And he did Moses just as he had commanded Yahweh him and he took Joshua and he made stand him before Eleazar the priest and before all the congregation.
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
23 And he laid hands his on him and he commissioned him just as he had spoken Yahweh by [the] hand of Moses.
Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.

< Numbers 27 >