< Numbers 20 >

1 And they came [the] people of Israel all the congregation [the] wilderness of Zin in the month first and it remained the people in Kadesh and she died there Miriam and she was buried there.
Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.
2 And not it belonged water to the congregation and they assembled on Moses and on Aaron.
Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni.
3 And it quarreled the people with Moses and they said saying and if we had died when died brothers our before Yahweh.
Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana!
4 And why? have you brought [the] assembly of Yahweh into the wilderness this to die there we and livestock our.
Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu?
5 And why? have you brought up us from Egypt to bring us to the place the evil this not - a place of seed and fig tree and vine and pomegranate and [is] water there not to drink.
Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”
6 And he went Moses and Aaron from before the assembly to [the] entrance of [the] tent of meeting and they fell on faces their and it appeared [the] glory of Yahweh to them.
Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea.
7 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Bwana akamwambia Mose,
8 Take the rod and assemble the congregation you and Aaron brother your and you will speak to the rock to eyes their and it will give water its and you will bring out for them water from the rock and you will give drink to the congregation and livestock their.
“Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”
9 And he took Moses the rod from to before Yahweh just as he had commanded him.
Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza.
10 And they made assemble Moses and Aaron the assembly to [the] face of the rock and he said to them listen please O rebels ¿ from the rock this will we bring out for you water.
Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?”
11 And he raised Moses hand his and he struck the rock with rod his two times and they came out waters many and it drank the congregation and livestock their.
Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.
12 And he said Yahweh to Moses and to Aaron because not you believed me to treat as holy me to [the] eyes of [the] people of Israel therefore not you will bring the assembly this into the land which I have given to them.
Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”
13 They [were] [the] waters of Meribah where they quarreled [the] people of Israel with Yahweh and he showed himself holy among them.
Haya yalikuwa maji ya Meriba, mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.
14 And he sent Moses messengers from Kadesh to [the] king of Edom thus he says brother your Israel you you know all the hardship which it has come upon us.
Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema: “Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata.
15 And they went down ancestors our Egypt towards and we dwelt in Egypt days many and they did harm to us Egypt and to ancestors our.
Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu,
16 And we cried out to Yahweh and he heard voice our and he sent an angel and he brought out us from Egypt and here! we [are] in Kadesh city of [the] outskirt[s] of territory your.
lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri. “Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako.
17 Let us pass please in land your not we will pass in a field and in a vineyard and not we will drink water of a well [the] way of the king we will go not we will turn aside right and left until that we will pass through territory your.
Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”
18 And it said to him Edom not you will pass in me lest with the sword I should come out to meet you.
Lakini mfalme wa Edomu akajibu: “Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”
19 And they said to him [the] people of Israel on the highway we will go up and if waters your we will drink I and livestock my and I will give price their only there not [is] a thing on feet my let me pass through.
Waisraeli wakajibu: “Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”
20 And it said not you will pass through and it came out Edom to meet him with a people massive and with a hand strong.
Watu wa Edomu wakajibu tena: “Hamwezi kupita hapa.” Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu.
21 And it refused - Edom to permit Israel to pass in territory its and it turned aside Israel from on it.
Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.
22 And they set out from Kadesh and they came [the] people of Israel all the congregation Hor the mountain.
Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori.
23 And he said Yahweh to Moses and to Aaron at Hor the mountain on [the] border of [the] land of Edom saying.
Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni,
24 He will be gathered Aaron to people his for not he will go into the land which I have given to [the] people of Israel on that you rebelled against mouth my to [the] waters of Meribah.
“Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba.
25 Take Aaron and Eleazar son his and bring up them Hor the mountain.
Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori.
26 And strip off Aaron garments his and you will clothe with them Eleazar son his and Aaron he will be gathered and he will die there.
Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”
27 And he did Moses just as he had commanded Yahweh and they went up to Hor the mountain to [the] eyes of all the congregation.
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli.
28 And he stripped off Moses Aaron garments his and he clothed with them Eleazar son his and he died Aaron there at [the] top of the mountain and he went down Moses and Eleazar from the mountain.
Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
29 And they saw all the congregation that he had died Aaron and they wept for Aaron thirty day[s] all [the] house of Israel.
Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.

< Numbers 20 >