< Numbers 15 >

1 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
2 Speak to [the] people of Israel and you will say to them that you will go into [the] land of dwelling places your which I [am] about to give to you.
“Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
3 And you will make a fire offering to Yahweh a burnt offering or a sacrifice to fulfill a vow or a freewill offering or at appointed feasts your to make an odor of soothing to Yahweh from the herd or from the flock.
mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
4 And he will bring near the [one who] brings near offering his to Yahweh a grain offering fine flour one tenth [of an ephah] mixed with [the] fourth of hin oil.
Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
5 And wine for the drink offering fourth of hin you will offer with the burnt offering or for the sacrifice for the lamb one.
Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
6 Or for the ram you will offer a grain offering fine flour two tenths [of an ephah] mixed with oil third of hin.
Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
7 And wine for the drink offering third of hin you will bring near an odor of soothing to Yahweh.
Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
8 And if you will offer a young one of cattle a burnt offering or a sacrifice to fulfill a vow or peace offerings to Yahweh.
Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
9 And he will bring near with [the] young one of cattle a grain offering fine flour three tenths [of an ephah] mixed with oil half of hin.
Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
10 And wine you will bring near for the drink offering half of hin a fire offering of an odor of soothing to Yahweh.
Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
11 Thus it will be done for the bull one or for the ram one or for the small livestock among the lambs or among the kids.
Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
12 According to the number which you will offer thus you will do for the one according to number their.
Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
13 Every native-born he will do thus these [things] to bring near a fire offering of an odor of soothing to Yahweh.
Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
14 And if he will sojourn with you a sojourner or [one] who [is] among midst of you to generations your and he will offer a fire offering of an odor of soothing to Yahweh just as you do so he will do.
Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
15 The assembly a statute one [will belong] to you and to the sojourner who sojourns a statute of perpetuity to generations your as you as the sojourner it will be before Yahweh.
Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
16 A law one and judgment one it will belong to you and to the sojourner who sojourns with you.
Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
17 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
18 Speak to [the] people of Israel and you will say to them when come you into the land where I [am] about to bring you there.
“Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
19 And it will be when eat you from [the] food of the land you will offer up a contribution to Yahweh.
mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
20 [the] first of Dough your a cake you will offer up a contribution like a contribution of [the] threshing floor so you will offer up it.
Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
21 Some of [the] first of dough your you will give to Yahweh a contribution to generations your.
Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
22 And if you will err and not you will observe all the commandments these which he has spoken Yahweh to Moses.
Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
23 All that he has commanded Yahweh to you by [the] hand of Moses from the day when he commanded Yahweh and onwards to generations your.
-kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
24 And it will be if away from [the] eyes of the congregation it was done to inadvertence and they will offer all the congregation a young bull a young one of cattle one to a burnt offering to an odor of soothing to Yahweh and grain offering its and drink offering its according to the ordinance and a male goat of goats one to a sin offering.
Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
25 And he will make atonement the priest on all [the] congregation of [the] people of Israel and it will be forgiven to them for [was] inadvertence it and they they have brought offering their a fire offering to Yahweh and sin offering their before Yahweh on inadvertence their.
Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
26 And it will be forgiven to all [the] congregation of [the] people of Israel and to the sojourner who sojourns in midst of them for to all the people by inadvertence.
Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
27 And if a person one it will sin by inadvertence and it will bring near a female goat a daughter of year its to a sin offering.
Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
28 And he will make atonement the priest on the person who has gone astray by sin by inadvertence before Yahweh to make atonement on him and it will be forgiven to him.
Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
29 The native-born among [the] people of Israel and to the sojourner who sojourns in midst of them a law one it will belong to you for the [one who] acts by inadvertence.
Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
30 And the person who it will act - with a hand raised one of the native-born and one of the sojourner[s] Yahweh he [is] blaspheming and it will be cut off the person that from [the] midst people its.
Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
31 For [the] word of Yahweh he has despised and commandment his he has broken certainly - it will be cut off the person that iniquity its [will be] on it.
Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
32 And they were [the] people of Israel in the wilderness and they found a man gathering wood on [the] day of the sabbath.
Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
33 And they brought near him the [ones who] found him gathering wood to Moses and to Aaron and to all the congregation.
Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
34 And they left him in custody for not it had been decided what? will it be done to him.
Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
35 And he said Yahweh to Moses certainly he will be put to death the man it will stone him with stones all the congregation from [the] outside of the camp.
Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
36 And they brought out him all the congregation to from [the] outside of the camp and they stoned him with stones and he died just as he had commanded Yahweh Moses.
Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
37 And he said Yahweh to Moses saying.
BWANA akanena na Musa tena, akasema,
38 Speak to [the] people of Israel and you will say to them and they will make for themselves tassel[s] on [the] corners of clothes their to generations their and they will put on [the] tassel[s] of the corner a cord of violet stuff.
“Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
39 And it will become for you tassel[s] and you will see it and you will remember all [the] commandments of Yahweh and you will observe them and not you will go about after own heart your and after own eyes your which you [are] acting as prostitutes after them.
Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
40 So that you may remember and you will observe all commandments my and you will be holy to God your.
Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
41 I [am] Yahweh God your who I brought out you from [the] land of Egypt to become for you God I [am] Yahweh God your.
Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”

< Numbers 15 >