< Nahum 1 >

1 [the] oracle of Nineveh [the] document of [the] vision of Nahum the Elkoshite.
Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
2 [is] a God Jealous and avenging Yahweh [is] avenging Yahweh and a lord of rage [is] avenging Yahweh to opponents his and [is] maintaining he to enemies his.
Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
3 Yahweh [is] long of anger (and great of *Q(K)*) power and certainly not he will leave unpunished Yahweh [is] in storm-wind and in storm way his and [is] cloud [the] dust of feet his.
Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
4 [he is] rebuking the Sea and he made dry it and all the rivers he dries up it withers Bashan and Carmel and [the] blossom of Lebanon it withers.
Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
5 Mountains they quake from him and the hills they melt and it lifted up the earth from before him and [the] world and all [those who] dwell in it.
Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
6 Before indignation his who? will he stand and who? will he endure at [the] burning of anger his rage his it is poured out like fire and the rocks they are pulled down from him.
Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
7 [is] good Yahweh a refuge in a day of trouble and [he is] knowing [those who] take refuge in him.
Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
8 And with a flood [which] passes over complete destruction he will make place its and enemies his he will pursue darkness.
lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
9 Whatever you will plot! against Yahweh complete destruction he [will be] making not it will arise two times trouble.
Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
10 For to thorns interwoven and like drink their drunkards they will be consumed like stubble dry full.
Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
11 From you he has come out [one who] plots on Yahweh evil a counselor of worthlessness.
Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
12 Thus - he says Yahweh though complete and thus numerous and thus they will be cut down and he will pass away and I have afflicted you not I will afflict you again.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
13 And now I will break yoke-bar his from on you and fetters your I will tear apart.
Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
14 And he has commanded on you Yahweh not it will be sown from name your again from [the] house of gods your I will cut off idol and molten image I will make grave your for you are insignificant.
Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
15 There! on the mountains [the] feet of [one who] bears news [one who] proclaims peace celebrate a festival O Judah festivals your pay vows your for not he will repeat again (to pass *Q(k)*) in you a worthless person all of him it will be cut off.
Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.

< Nahum 1 >