< Micah 3 >
1 And I said hear please O chiefs of Jacob and O rulers of [the] house of Israel ¿ not [belong] to you [does] to know justice.
Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
2 Haters of good and lovers of (evil *Q(K)*) tearers away of skin their from on them and flesh their from on bones their.
ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
3 And [those] who they have eaten [the] flesh of people my and skin their from on them they have stripped off and bones their they have broken in pieces and they have chopped [them] up just as in the pot and like meat in [the] midst of a caldron.
ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
4 Then they will cry out to Yahweh and not he will answer them and he will hide face his from them at the time that since they have made evil deeds their.
Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
5 Thus he says Yahweh on the prophets who mislead people my who bite with teeth their and they proclaim peace and [the one] who not he puts on mouth their and they consecrate on him war.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
6 Therefore night [will belong] to you from vision and it will grow dark to you from divining and it will go the sun on the prophets and it will be dark on them the day.
Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
7 And they will be ashamed the seers and they will be abashed those [who] divine and they will cover over a moustache all of them for there not [will be] an answer of God.
Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
8 And but I I am full power with [the] spirit of Yahweh and justice and might to declare to Jacob transgression its and to Israel sin its.
Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 Hear please this O chiefs of [the] house of Jacob and O rulers of [the] house of Israel who loathe justice and every straight [thing] they make crooked.
Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
10 [who] build Zion with blood and Jerusalem with injustice.
mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Chiefs its - for a bribe they judge and priests its for a price they teach and prophets its for money they divine and on Yahweh they depend saying ¿ not [is] Yahweh in midst our not it will come on us calamity.
Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
12 Therefore on account of you Zion a field it will be plowed and Jerusalem heaps of ruins it will be and [the] mountain of the house high places of a forest.
Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.