< Matthew 18 >

1 In that [very] hour came the disciples to Jesus saying; Who then [the] greatest is in the kingdom of the heavens?
Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
2 And having called to [Him] (Jesus *k*) a child He set it in midst of them
Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
3 and said; Amen I say to you; only unless you may turn and may become as the little children, certainly not shall you enter into the kingdom of the heavens.
Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
4 Whoever therefore (will humble *N(k)O*) himself as little child this, he is the greater in the kingdom of the heavens.
Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
5 And who[ever] (if *NK(o)*) shall receive one little child (such *N(k)O*) in the name of Me, Me myself receives.
“Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
6 Who[ever] then maybe may cause to stumble one of the little ones of these who are believing in Me myself, it is better for him that may be hung a millstone heavy (around *N(k)(o)*) the neck of him, and he may be sunk in the depth of the sea.
Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
7 Woe to the world because of the causes of sin; Necessary [are] for (is *ko*) to come the stumbling blocks, but woe to the man (that [one] *k*) through whom the offense comes!
“Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
8 If now the hand of you or the foot of you causes to sin you, do cut off (it *N(K)O*) and do cast [it] from you; better for you it is to enter into life crippled or lame than two hands or two feet having to be cast into the fire eternal. (aiōnios g166)
Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
9 And if the eye of you causes to sin you, do gouge out it and do cast [it] from you; better for you it is one-eyed into life to enter than two eyes having to be cast into the hell of the fire. (Geenna g1067)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
10 do see [that] not may you despise one of the little ones of these; I say for to you that the angels of them in [the] heavens through all [times] behold the face of the Father of mine who [is] in [the] heavens.
“Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
11 (came *KO*) (for son of man to save those already perishing. *K*)
Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
12 What you do think? If may happen a certain man [has] a hundred sheep and shall have gone astray one of them, surely (he will leave *N(k)O*) the ninety nine on the mountains, (and *no*) having gone will seek the [one] going astray?
“Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
13 And if he may happen to find it, Amen I say to you that he rejoices over it more than over the ninety nine which not gone astray.
Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
14 Thus not it is [the] will of the Father (of you *NK(O)*) who [is] in [the] heavens that may perish (one *N(k)O*) of the little ones of these.
Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
15 If now shall sin against you the brother of you, do go (and *k*) do reprove him between you and him alone. If you he shall hear, you have gained the brother of you.
“Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
16 only however unless he shall hear, do take with you more one or two that upon [the] testimony of two witnesses or of three may be strengthened every declaration.
Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
17 If now he shall fail to listen to them, do tell [it] to the church. If now also to the church he shall fail to listen, he should be to you as the pagan and the tax collector.
Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
18 Amen I say to you; as much as (if *NK(o)*) you shall bind on the earth, will have been bound in (*ko*) heaven; and as much as if you shall loose on the earth, will have been loosed in (*ko*) heaven.
“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
19 Again (Amen *NO*) I say to you that if two shall agree (of *no*) you on the earth concerning any matter that if they shall ask, it will be done for them by the Father of Mine who [is] in [the] heavens.
“Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
20 Where for are two or three assembled unto My name, there am I in [the] midst of them.
Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
21 Then having come Peter said to Him; Lord, how often will sin against me myself the brother of mine and I will forgive him? Up to seven times?
Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
22 Says to him Jesus; Not I say to you up to seven times but up to seventy times seven!
Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Because of this has become like the kingdom of the heavens to a man a king who desired to settle accounts with the servants of him.
“Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
24 When was beginning then he to settle (was brought to *NK(o)*) to him one a debtor of ten thousand talents.
Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
25 [When] not is having [anything] now he to pay he commanded him the master (of him *k*) to be sold and the wife (of him *ko*) and the children and all as much as (he has *N(k)O*) and payment to be made.
Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
26 Having fallen down therefore the servant was bowing on his knees to him saying; (lord *ko*) do have patience with (me myself, *NK(o)*) and all I will pay to you.
“Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
27 Having been moved with compassion now the master of the servant, that [one] released him and the debt forgave him.
Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
28 Having gone out however the servant same found one of the fellow servants of him who was owing to him a hundred denarii, and having seized him he was throttling [him] saying; do pay (to me *k*) (if *N(k)O*) any you owe.’
“Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
29 Having fallen down therefore the fellow servant of him (into the feet of him *K*) was begging him saying; do have patience with (me myself, *NK(o)*) and (all things *K*) I will pay you.
“Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
30 But not he was willing, but having gone he cast him into prison until (what of him *ko*) he may pay that which is being owed.
“Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
31 Having seen (therefore *N(k)O*) the fellow servants of him the [things] having taken place they were grieved deeply, and having gone they narrated to the master (of themselves *N(k)O*) all that having taken place.
Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
32 Then having called to him the master of him says to him; Servant evil, all the debt, that [one] I forgave you because you begged me.
“Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
33 Surely it was necessary also you to have pitied the fellow servant of you as also I myself also I myself you pitied?
Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
34 And having been angry the master of him delivered him to the jailers until that he may pay all which is being owed (to him. *ko*)
Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
35 Thus also the Father of Mine (heavenly *N(k)O*) will do to you only unless you may forgive each the brother of him from the heart of you (the trespasses of them. *K*)
“Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”

< Matthew 18 >