< Mark 3 >
1 And He entered again into the synagogue, and there was there a man withered having the hand,
Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
2 and they were watching Him whether on the Sabbaths He will heal him in order that (they may accuse *NK(o)*) Him.
Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
3 And He says to the man the (withered *N(k)O*) hand having: (do arise *N(k)O*) into the midst.
Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
4 And He says to them; Is it lawful on the Sabbaths good to do or to do evil? Life to save or to kill? But they were silent.
Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
5 And having looked around on them with anger, being grieved at the hardness of the heart of them, He says to the man; do stretch out the hand (of you. *KO*) And he stretched [it] out, and was restored the hand of him (sound as another. *K*)
Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
6 And having gone out the Pharisees immediately with the Herodians counsel (were giving *N(k)O*) against Him how Him they may destroy.
Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
7 And Jesus with the disciples of Him withdrew to the sea, and great a multitude from Galilee (followed *N(k)O*) (him *k*) and from Judea
Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
8 and from Jerusalem and from Idumea and beyond the Jordan and (*k*) around Tyre and Sidon, A multitude great (having heard *N(k)O*) as much as (He was doing *NK(o)*) came to Him.
Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
9 And He spoke to the disciples of Him that a boat may wait upon Him on account of the crowd that not they may press upon Him.
Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
10 Many for He healed so as for to press upon Him that Him they may touch as many as had diseases.
Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
11 And the spirits unclean, whenever Him (they were seeing they were falling down *N(k)O*) before Him and (they were crying out saying *N(k)O*) that You yourself are the Son of God.
Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
12 And much He was rebuking them so that not Him known (they may make. *NK(o)*)
Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
13 And He goes up on the mountain and calls near those whom he was wanting Himself, and they went to Him.
Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
14 And He appointed twelve (whom also apostles He called [them] *NO*) that they may be with Him and that He may send them to preach
Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
15 and to have authority (to heal diseases and *K*) to cast out demons.
na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
16 (And He appointed the Twelve *NO*) And He added [the] name to Simon Peter,
Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
17 and James the [son] of Zebedee and John the brother of James, and He added to them [the] (names *NK(o)*) Boanerges, which is Sons of thunder;
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
18 and Andrew and Philip and Bartholomew and Matthew and Thomas and James the [son] of Alphaeus and Thaddaeus and Simon the Zealot
Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 and Judas Iscariot who also betrayed Him. And (He comes *N(K)O*) to a house,
na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
20 and comes together again (*no*) a crowd so that not to be able they (even *N(k)O*) bread to eat.
Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
21 And having heard [of it] those belonging to Him went out to seize Him; they were saying for that He is crazy.
Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
22 And the scribes those from Jerusalem having come down were saying that Beelzebul He has and that By the prince of the demons He casts out the demons.
Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
23 And having called to [Him] them in parables He was speaking to them: How is able Satan Satan to cast out?
Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
24 And if a kingdom against itself shall be divided, not is able to stand the kingdom that;
Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 And if a house against itself shall be divided, not (will be able *N(k)O*) house that (to stand; *NK(o)*)
Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 And if Satan has risen up against himself and (was divided, *N(k)O*) not he is able (to stand *N(k)O*) but an end is coming to.
Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
27 (But *NO*) not is able no [one] into the house of the strong man having entered the goods of him to plunder, only unless first the strong man he shall bind, And then the house of him (he will plunder. *NK(o)*)
Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
28 Amen I say to you that all will be forgiven to the sons of men the sins and (the *no*) blasphemies (as much as if *N(k)O*) they shall have blasphemed;
Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
29 Who[ever] however maybe may blaspheme against the Spirit Holy not has forgiveness to the age, but guilty is [of] eternal (sin; *N(K)O*) (aiōn , aiōnios )
Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
30 For they were saying; A spirit unclean he has.
Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
31 (And he comes *N(K)O*) the mother of Him and the brothers of Him. and outside (standing *N(k)O*) sent to Him (calling *N(k)O*) Him.
Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
32 And was sitting around Him a crowd (And *no*) (they speak *N(k)O*) (now *k*) to Him; Behold the mother of You and the brothers of You (and the sisters of you *NO*) outside are seeking You.
Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
33 And (answering *N(k)O*) them (He says; *N(k)O*) Who are the mother of Mine (and *N(k)O*) the brothers of Mine?
Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
34 And having looked around on those who around Him surrounding were sitting He says; Behold the mother of Mine and the brothers of Mine!
Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 Who[ever] for maybe may do the will of God, he brother of Mine and sister (of Mine *k*) and mother is.
Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”