< Leviticus 22 >
1 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Yahweh akazungumza na Musa, kusema,
2 Speak to Aaron and to sons his so they may separate themselves from [the] holy things of [the] people of Israel and not they will profane [the] name of holiness my which they [are] setting apart as holy to me I [am] Yahweh.
“Ongea na Aroni na wanawe, waambie wajiepushe na vitu vitakatifu vya watu wa Israeli wanavyovitenga kwangu. Wasilinajisi jina langu. Mimi ndimi Yahweh.
3 Say to them to generations your every man - who he will draw near from all offspring your to the holy things which they will set apart as holy [the] people of Israel to Yahweh and uncleanness his [is] on him and it will be cut off the person that from to before me I [am] Yahweh.
Waambie, 'Ikiwa mmoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote anakaribia vitu vitakatiifu vile ambavyo watu wa Israeli wamevitenga kwa Yahweh, wakati akiwa najisi, sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu. Mimi ndimi Yahweh.
4 A man a man from [the] offspring of Aaron and he [is] having a serious skin disease or [is] discharging in the holy things not he will eat until that he will be pure and who [-ever] touches any [thing] unclean of a corpse or anyone whom it will go out from him a laying of seed.
Hatakuwapo yeyote wa uzao wa Aroni aliye na ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza, au maambukizi yatirirkayo kutoka mwilini mwake, atakayekula sehemu yoyote ya dhabihu inatolewayo kwa Yahweh mpaka atakapotakasika. Yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi kwa njia ya kugusa maiti, au kwa kumgusa mtu yeyote aliyetokwa na shahawa,
5 Or anyone who he will touch any swarming thing which it is unclean to him or anyone who he is unclean to him to all uncleanness his.
au yeyote agusaye mnyama atakayemtia unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya najisi, kwa hiyo unajisi wowote unaweza kuwa—
6 Anyone who it will touch it and it will be unclean until the evening and not he will eat any of the holy things that except he has washed body his with water.
kuhani yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi hata jioni. Hatakula chochote cha vitu vitakatifu, isipokuwa ameuosha mwili wake katika maji.
7 And it will go the sun and he will be clean and after he will eat any of the holy things for [is] food his it.
Jua linapotua, ndipo atakuwa safi. Baada ya machweo anaweza kula kutoka katika vitu vitakatifu, kwasababu hivyo ni vyakuala vyake.
8 A carcass and a torn animal not he will eat to become unclean by it I [am] Yahweh.
Asile mzoga wowote uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori, ambaye kwake atajitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh.
9 And they will keep duty my and not they will bear on it sin and they will die by it for they will profane it I [am] Yahweh [who] sets apart as holy them.
Ni lazima makuhani wafuate maagizo yangu, ama sivyo watakuwa na hatia ya dhambi na wangeweza kufa kwa kunitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh ninayewafanya wao watakatifu.
10 And any stranger not he will eat a holy thing a resident alien of a priest and a hired laborer not he will eat a holy thing.
Hakuna mtu kutoka nje ya familia ya kuahani, wakiwemo wageni wa kuhani au watumwa wake wa kuajiliwa, atakayeweza kula kitu chochote kilicho kitakatifu.
11 And a priest if he will acquire a person [the] acquisition of money his he he will eat in it and [the] one born of household his they they will eat in food his.
Lakini kama huyo kuhani amenunua mtumwa kwa fedha yake mwenyewe, mtumwa huyo anaweza kula kutoka katika vitu vilivyotengwa kwa Yahweh. Na watu wa familia ya kuhani na watumwa waliozaliwa nyumbani mwake, pia wanaweza kula pamoja naye kutoka katika vitu hivyo.
12 And a daughter of a priest if she will belong to a man strange she in [the] contribution of the holy things not she will eat.
Ikiwa binti wa kuhani ameolewa na mtu asiye kuhani, hataweza kula chochote cha mchango wa matoleo matakatifu.
13 And a daughter of a priest if she will be a widow and a divorced [woman] and offspring not [belongs] to her and she will return to [the] house of father her like youth her any of [the] food of father her she will eat and any stranger not he will eat in it.
Lakini ikiwa huyo binti wa kuhani ni mjane au ametalikiwa, na ikiwa hana mtoto, na anarudi kuishi knyumbani kwa baba yake kama alivyokuwa wakati wa ujana wake, anaweza kula kutoka katika chakula cha baba yake. Lakini hakuna yeyote asiye wa familia ya kikuhani anatakayeruhusiwa kula kutoka katika chakula cha kuhani.
14 And anyone if he will eat a holy thing by inadvertence and he will add fifth its to it and he will give to the priest the holy thing.
Kama mtu anakula chakula kitakatifu bila ya kukijua, naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake na kukirejesha kwa kuhani.
15 And not they will profane [the] holy things of [the] people of Israel which they will lift up to Yahweh.
Haiwapasi watu wa Israeli kutoheshimu vitu vitakatifu ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa kwa Yahweh,
16 And they will cause to bear them iniquity of guilt when eat they holy things their for I [am] Yahweh [who] sets apart as holy them.
kisha wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia ya kula chakula kitakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Yahweh awafanyaye wao watakatifu.”
17 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Yahweh akazungumza na Musa, akasema,
18 Speak to Aaron and to sons his and to all [the] people of Israel and you will say to them a person a person from [the] house of Israel and of the sojourner[s] in Israel who he will present present his for all vows their and for all freewill offerings their which they will present to Yahweh to a burnt offering.
“Sema na Aroni na wanawe, na kwa watu wa Israeli wote. Waambie, Mwisraeli yeyote, au Mgeni anayeishi katika Israeli, waletapo dhabihu—iwe ni kutimiza kiapo, au iwe ni sadaka ya hiari, au wanaleta kwa Yahweh sadaka ya kuteketezwa kwa moto,
19 For acceptance your unblemished a male among the cattle among the young rams and among the goats.
ikiwa wanataka ikubalike, ni lazima watowe mnyama dume asiye na dosari, kutoka kwenye kundi la ng'ombe, kondoo au mbuzi
20 All that [is] in it a blemish not you will present for not for acceptance it will be of you.
Lakini hamtatoa chochote kilicho na dosari. Sitakipokea kwa niaba yenu.
21 And anyone if he will present a sacrifice of peace offering to Yahweh to fulfill a vow or to a freewill offering in the herd or in the flock unblemished it will be for acceptance any blemish not it will be in it.
Yeyote atoae dhabihu ya sadaka ya ushirika kutoka katika kundi la ng'ombe au la kondoo kwa Yahweh ili kutimiza kiapo, au kama sadaka ya hiari, ili ikubalike, ni lazima isiwe na kilema. Ni lazima pasiweko na kasoro katika mnyama.
22 Blindness or a fracture or a mutilation or a wart or eczema or scabs not you will present these to Yahweh and a fire offering not you must give any of them on the altar to Yahweh.
Msitoe kabisa wanyama waliovipofu, waliojeruhiwa, wala walio na kilema, wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga. Msiwatoe hawa kuwa dhabihu ya kuteketezwa kwa moto iliyotolewa kwa Yahweh juu ya madhabahu.
23 And an ox and a sheep [having] something enlarged and [having] something stunted a freewill offering you will offer it and for a vow not it will be accepted.
Unaweza kumleta makisai au mwana-kondoo mlemavu au aliyedumaa kuwa sadaka ya hiari, lakini sadaka kama hiyo kwa ajili kutimiza kiapo, haitapokelewa.
24 And [one which] is squashed and [one which] is crushed and [one which] is torn and [one which] is cut not you will present to Yahweh and in land your not you will do [it].
Usitoe kwa Yahweh mnyama yeyote aliyetiwa jeraha, kupondwa, au kukatwa korodani zake.
25 And from [the] hand of a son of foreignness not you must present [the] food of God your any of all these [animals] for disfigurement their [is] in them a blemish [is] in them not they will be accepted for you.
Usifanye haya katika nchi yako. Usilete mkate wa Mungu wako kutoka mkononi mwa mgeni. Hao wanyama wenye vilema na dosari ndani yao, hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako.
26 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Yahweh akamwambia Musa na akasema,
27 An ox or a young ram or a goat if it will be born and it will be seven days under mother its and from [the] day eighth and onwards it will be accepted to a present of a fire offering to Yahweh.
“Wakati ndama, mwana—kondo au mwana—mbuzi azaliwapo, sharti abaki na mama yake kwa muda wa siku saba. Ndipo kuanzia siku ya nane na kuendelea, anaweza kupokelewa kuwa dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh.
28 And an ox or a sheep it and young its not you must cut [the] throat of in a day one.
Usimchinje ng'ombe jike pamoja na ndama wake au mbuzi jike pamoja na kitoto chake kwa siku moja.
29 And if you will sacrifice a sacrifice of thanksgiving to Yahweh for acceptance your you will sacrifice [it].
Utoapo sadaka ya shukrani kwa Yahweh utaitoa kwa njia iliyokubalika.
30 On the day that it will be eaten not you will leave over any of it until morning I [am] Yahweh.
Ni lazima iliwe siku iyo hiyo inayotolewa. Hutakiwi kubakiza chochote hata asubuhi. Mimi ndimi Yahweh.
31 And you will keep commandments my and you will do them I [am] Yahweh.
Kwa hiyo imewapasa kuzishika amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Yahweh.
32 And not you will profane [the] name of holiness my and I will show myself holy in among [the] people of Israel I [am] Yahweh [who] sets apart as holy you.
Msiliabishe jina langu takatifu. Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli. Mimi ndimi Yahweh niwafanyaye ninyi watakatifu,
33 Who brought out you from [the] land of Egypt to become for you God I [am] Yahweh.
ambaye amewaleta kutoka katika nchi ya Misri ili niwe Mungu wenu: Mimi ndimi Yahweh.”