< Judges 4 >

1 And they repeated [the] people of Israel to do the evil in [the] eyes of Yahweh and Ehud he had died.
Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni pa Bwana.
2 And he sold them Yahweh in [the] hand of Jabin [the] king of Canaan who he reigned in Hazor and [was] [the] commander of army his Sisera and he [was] dwelling in Harosheth Haggoyim.
Hivyo Bwana akawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu
3 And they cried out [the] people of Israel to Yahweh for nine hundred chariot[s] of iron [belonged] to him and he he oppressed [the] people of Israel with force twenty year[s].
Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli wakamlilia Bwana wakaomba msaada.
4 And Deborah a woman a prophetess [the] wife of Lappidoth she [was] judging Israel at the time that.
Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye alikuwa anaamua Israeli wakati ule.
5 And she [was] dwelling under [the] palm tree of Deborah between Ramah and between Beth-el in [the] hill country of Ephraim and they went up to her [the] people of Israel for judgment.
Debora alikuwa akiketi chini ya Mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama na Betheli katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakaja kwake ili awaamue.
6 And she sent and she summoned Barak [the] son of Abinoam from Kedesh Naphtali and she said to him ¿ not has he commanded - Yahweh [the] God of Israel go and you will march at [the] mountain of Tabor and you will take with you ten thousand man from [the] descendants of Naphtali and of [the] descendants of Zebulun.
Akatuma wamwite Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali na kumwambia, “Bwana, Mungu wa Israeli, anakuagiza: ‘Nenda, chukua wanaume 10,000 toka Naftali na Zabuloni, mwende Mlima Tabori.
7 And I will draw to you to [the] wadi of Kishon Sisera [the] commander of [the] army of Jabin and chariotry his and multitude his and I will give him in hand your.
Nitamshawishi Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake na jeshi lake, hadi Mto Kishoni na kumtia mikononi mwako.’”
8 And he said to her Barak if you will go with me and I will go and if not you will go with me not I will go.
Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami nitakwenda, lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”
9 And she said certainly I will go with you nevertheless for not it will be honor your on the way which you [are] going for in [the] hand of a woman he will sell Yahweh Sisera and she rose Deborah (and she went *L(abh)*) with Barak Kedesh towards.
Debora akamwambia, “Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini njia unayoiendea haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.” Hivyo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi,
10 And he summoned Barak Zebulun and Naphtali Kedesh towards and it went up at feet his ten thousand man and she went up with him Deborah.
mahali ambapo Baraka aliwaita Zabuloni na Naftali. Watu 10,000 wakamfuata Baraka, na Debora pia akaenda pamoja naye.
11 And Heber the Kenite [was] separate from [the] Kenite[s] from [the] descendants of Hobab [the] father-in-law of Moses and he had pitched tent his to [the] great tree (in Zaanannim *Q(K)*) which [is] with Kedesh.
Basi Heberi, Mkeni, alikuwa amejitenga na Wakeni wengine, yaani, wazao wa Hobabu, mkwewe Mose, naye akapiga hema lake karibu na ule mti mkubwa wa mwaloni ulioko Saananimu, karibu na Kedeshi.
12 And people told to Sisera that he had gone up Barak [the] son of Abinoam [the] mountain of Tabor.
Sisera alipoambiwa kuwa Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa amepanda Mlima Tabori,
13 And he summoned Sisera all chariotry his nine hundred chariot[s] of iron and all the people which [was] with him from Harosheth Haggoyim to [the] wadi of Kishon.
Sisera akakusanya pamoja magari yake yote 600 ya chuma na watu wote waliokuwa pamoja naye, kuanzia Haroshethi-Hagoyimu mpaka Mto wa Kishoni.
14 And she said Deborah to Barak arise for this [is] the day which he has given Yahweh Sisera in hand your ¿ not Yahweh has he gone out before you and he went down Barak from [the] mountain of Tabor and ten thousand man [were] after him.
Ndipo Debora akamwambia Baraka, “Nenda! Hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera mikononi mwako. Je, Bwana hakukutangulia mbele yako?” Hivyo Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori, akifuatwa na watu 10,000.
15 And he routed Yahweh Sisera and all the chariotry and all the army to [the] mouth of [the] sword before Barak and he went down Sisera from on the chariot and he fled on feet his.
Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, pamoja na jeshi lake lote kwa upanga mbele ya Baraka, naye Sisera akaliacha gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 And Barak he pursued after the chariotry and after the army to Harosheth Haggoyim and it fell all [the] army of Sisera to [the] mouth of [the] sword not it was left up to one.
Lakini Baraka akafuata magari pamoja na jeshi mpaka Haroshethi-Hagoyimu. Jeshi lote la Sisera likaanguka kwa upanga, wala hakuna hata mtu mmoja aliyesalia.
17 And Sisera he fled on feet his to [the] tent of Jael ([the] wife of *L(abh)*) Heber the Kenite for peace [was] between Jabin [the] king of Hazor and between [the] house of Heber the Kenite.
Sisera, hata hivyo, akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli, mkewe Heberi, Mkeni, kwa sababu palikuwa na uhusiano wa kirafiki kati ya Yabini mfalme wa Hazori na ukoo wa Heberi, Mkeni.
18 And she went out Jael to meet Sisera and she said to him turn aside! O lord my turn aside! to me may not you be afraid and he turned aside to her the tent towards and she covered him with the covering.
Yaeli akaenda kumlaki Sisera na kumwambia, “Karibu, bwana wangu, karibu ingia ndani kabisa. Usiogope.” Basi Sisera akaingia ndani ya hema ya Yaeli, naye akamfunika kwa blanketi nene.
19 And he said to her give to drink me please a little of water for I am thirsty and she opened [the] skin-bottle of milk and she gave a drink him and she covered him.
Akamwambia, “Nina kiu, tafadhali nipe maji ya kunywa.” Ndipo akafungua kiriba cha maziwa na kumpa akanywa, kisha akamfunika.
20 And he said to her stand [the] opening of the tent and it will be if anyone he will come and he will ask you and he will say ¿ [is] there here anyone and you will say no.
Naye Sisera akamwambia, “Simama mlangoni pa hema na mtu yeyote akija na kukuuliza, ‘Je, kuna mtu yeyote hapa?’ sema, ‘Hapana.’”
21 And she took Jael [the] wife of Heber [the] peg of the tent and she put the hammer in hand her and she went to him in secrecy and she drove the peg in temple his and it went down in the ground and he [was] sleeping and he was weary and he died.
Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akachukua nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akiwa amelala usingizi, akiwa amechoka. Akakigongomea kile kigingi kwenye paji la uso wake, kikapenya hata kuingia ardhini, naye akafa.
22 And there! Barak [was] pursuing Sisera and she went out Jael to meet him and she said to him come and I will show you the man whom you [are] seeking and he went to her and there! Sisera [was] lying dead and the peg [was] in temple his.
Baraka akakaribia akimfuatia Sisera, Yaeli akatoka kumlaki. Akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Hivyo wakaingia ndani ya hema wakiwa wamefuatana na tazama Sisera alikuwa amelala humo, akiwa amekufa, na hicho kigingi cha hema kikiwa kimegongomewa kupitia paji la uso wake.
23 And he subdued God on the day that Jabin [the] king of Canaan before [the] people of Israel.
Basi siku ile Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani, mbele ya Israeli.
24 And it went [the] hand of [the] people of Israel going and hard on Jabin [the] king of Canaan until that they cut off Jabin [the] king of Canaan.
Nao mkono wa Waisraeli ukaendelea kuwa na nguvu zaidi na zaidi dhidi ya Yabini, mfalme wa Kanaani, mpaka wakamwangamiza.

< Judges 4 >