< Judges 19 >

1 And it was in the days those and [was] a king there not in Israel and he was - a man a Levite sojourning in [the] remotest parts of [the] hill country of Ephraim and he took for himself a woman a concubine from Beth-lehem Judah.
Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme. Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda.
2 And she was angry towards him concubine his and she went from with him to [the] house of father her to Beth-lehem Judah and she was there days four months.
Lakini suria wake akafanya ukahaba dhidi yake, naye akamwacha akarudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne,
3 And he arose husband her and he went after her to speak to heart her (to bring back her *Q(K)*) and servant his [was] with him and a pair of donkeys and she brought him [the] house of father her and he saw him [the] father of the young woman and he was glad to meet him.
mume wake akaenda kumsihi ili arudi. Alikwenda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha.
4 And he took hold on him father-in-law his [the] father of the young woman and he remained with him three days and they ate and they drank and they spent [the] night there.
Baba mkwe wake, yaani, baba yake yule msichana, akamzuia ili akae, hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila, wakinywa na kulala huko.
5 And it was on the day fourth and they rose early in the morning and he arose to go and he said [the] father of the young woman to son-in-law his sustain heart your a morsel of bread and after you will go.
Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kula kitu chochote, ndipo uweze kwenda.”
6 And they sat down and they ate [the] two of them together and they drank and he said [the] father of the young woman to the man be willing please and spend [the] night so it may be good heart your.
Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha nafsi yako.”
7 And he arose the man to go and he urged him father-in-law his and he turned back and he spent [the] night there.
Basi yule mtu alipotaka kuondoka baba wa yule msichana akamsihi, basi akabaki usiku ule.
8 And he rose early in the morning on the day fifth to go and he said - [the] father of the young woman sustain please heart your and delay until declines the day and they ate [the] two of them.
Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja mpaka mchana!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.
9 And he arose the man to go he and concubine his and servant his and he said to him father-in-law his [the] father of the young woman here! please it is sinking the day to become evening spend [the] night please here! to decline the day spend [the] night here so it may be good heart your and you will rise early tomorrow for journey your and you will go to tent your.
Basi wakati yule mtu alipoinuka aende zake, pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba wa yule msichana akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka mapema asubuhi na uende nyumbani kwako.”
10 And not he was willing the man to spend [the] night and he arose and he went and he came to opposite Jebus that [is] Jerusalem and [were] with him a pair of donkeys saddled and concubine his [was] with him.
Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kwenda mpaka Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikiwa, pamoja na suria wake.
11 They [were] near Jebus and the day it had gone down exceedingly and he said the servant to master his come! please so let us turn aside to [the] city of the Jebusite[s] this so we may spend [the] night in it.
Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”
12 And he said to him master his not we will turn aside to a city foreign who not [are] of [the] people of Israel they and we will pass on to Gibeah.
Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea mpaka tufike Gibea.”
13 And he said to servant his (come! *Q(K)*) so let us drew near at one of the places and we will spend [the] night in Gibeah or in Ramah.
Akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji mmojawapo.”
14 And they passed on and they went and it went for them the sun beside Gibeah which [belongs] to Benjamin.
Hivyo wakaendelea na safari, jua likachwea walipokaribia Gibea ambao ni mji wa Benyamini.
15 And they turned aside there to go to spend [the] night in Gibeah and he went and he sat in [the] open square of the city and not anyone [was] receiving them the house towards to spend [the] night.
Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.
16 And there! - a man old [was] coming from work his from the field in the evening and the man [was] from [the] hill country of Ephraim and he [was] sojourning in Gibeah and [the] men of the place [were] Ben-jaminites.
Jioni ile mtu mmoja mzee toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi za shamba.
17 And he lifted up eyes his and he saw the man who was traveling in [the] open square of the city and he said the man old where? are you going and from where? are you coming.
Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnakwenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”
18 And he said to him [are] passing we from Beth-lehem Judah to [the] remotest parts of [the] hill country of Ephraim [am] from there I and I went to Beth-lehem Judah and [the] house of Yahweh I [am] going and not anyone [was] receiving me the house towards.
Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu, ambako ndiko ninakoishi. Nilikwenda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninakwenda katika nyumba ya Bwana. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake.
19 And [are] both straw as well as fodder there for donkeys our and [are] also food and wine there for me and for maidservant your and for the servant with servants your there not [is] lack of any thing.
Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu na mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako, yaani mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliyefuatana naye. Hatuhitaji kitu chochote.”
20 And he said the man old peace [be] to you certainly all lack your [is] on me only in the open square may not you spend [the] night.
Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, msilale katika uwanja huu wa mji.”
21 And he brought him to house his (and he fed *Q(k)*) the donkeys and they washed feet their and they ate and they drank.
Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.
22 They [were] making good heart their and there! [the] men of the city men of sons of worthlessness they surrounded the house beating violently on the door and they said to the man [the] master of the house old saying bring out the man who he came to house your so we may know him.
Walipokuwa wakijiburudisha, watu waovu wa mji huo, wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema na yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mtu aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”
23 And he went out to them the man [the] master of the house and he said to them may [you] not O brothers my may not you do evil please after that he has come the man this may [you] not house my may not you do the disgraceful folly this.
Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mtu ni mgeni wangu msifanye jambo hili la aibu.
24 Here! daughter my the virgin and concubine his let me bring out please them and afflict them and do to them the good in view your and to the man this not you must do [the] thing of disgraceful folly this.
Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira na suria wa huyu mtu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mtu huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”
25 And not they were willing the men to listen to him and he took hold the man on concubine his and he brought [her] out to them outside and they knew her and they abused her all the night until the morning and they let go her (just as came up *Q(K)*) the dawn.
Lakini wale watu hawakumsikia. Hivyo yule mtu akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku ule kucha mpaka asubuhi. Kulipoanza kupambazuka wakamwachia aende.
26 And she came the woman to [the] turning of the morning and she fell [the] entrance of [the] house of the man where master her [was] there until the light.
Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.
27 And he arose master her in the morning and he opened [the] doors of the house and he went out to go to way his and there! the woman concubine his [was] falling [the] entrance of the house and hands her [were] on the threshold.
Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameanguka pale penye ingilio la nyumba na mikono yake ikiwa penye kizingiti cha chini.
28 And he said to her get up so let us go and there not [was one who] answered and he took her on the donkey and he arose the man and he went to place his.
Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua akampandisha juu ya punda wake, wakaondoka kwenda nyumbani.
29 And he came to house his and he took the knife and he took hold on concubine his and he cut in pieces her to bones her into two [plus] ten pieces and he sent out her in all [the] territory of Israel.
Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, sehemu kumi na mbili, na kuvipeleka hivyo vipande katika sehemu zote za Israeli.
30 And it was every [one who] saw and he said not it has occurred and not it has been seen like this from [the] day came up [the] people of Israel from [the] land of Egypt until the day this set for yourselves on it take counsel and speak.
Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Israeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”

< Judges 19 >