< Jonah 1 >

1 And it came [the] word of Yahweh to Jonah [the] son of Amittai saying.
Neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amitai:
2 Arise go to Nineveh the city great and call out on it for it has come up wickedness their before me.
“Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”
3 And he arose Jonah to flee Tarshish towards from to before Yahweh and he went down Joppa and he found a ship - [which was] about to go Tarshish and he gave fare its and he went down in it to go with them Tarshish towards from to before Yahweh.
Lakini Yona alimkimbia Bwana na kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbia Bwana.
4 And Yahweh he threw a wind great to the sea and it was a storm great on the sea and the ship it thought to be broken.
Ndipo Bwana akatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika.
5 And they were afraid the sailors and they cried for help everyone to gods his and they threw the vessels which [were] in the ship into the sea to lighten from on them and Jonah he had gone down into [the] innermost parts of the ship and he had lain down and he had fallen fast asleep.
Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito. Lakini Yona alikuwa ameteremkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito.
6 And he drew near to him [the] chief of the sailor[s] and he said to him what? [is] to you sleeping arise call to god your perhaps he will give thought the god to us and not we will perish.
Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”
7 And they said each to neighbor his come so let us cast lots so we may know by which of whom? the evil this [belongs] to us and they cast lots and it fell the lot on Jonah.
Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.
8 And they said to him tell! please to us because of whom? the evil this [belongs] to us what? [is] occupation your and from where? do you come what? [is] land your and where? from this people [are] you.
Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”
9 And he said to them [am] a Hebrew I and Yahweh [the] God of the heavens I [am] fearing who he made the sea and the dry land.
Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabudu Bwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”
10 And they feared the men a fear great and they said to him what? this have you done for they knew the men that from to before Yahweh he [was] fleeing for he had told to them.
Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza, “Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbia Bwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)
11 And they said to him what? will we do to you so it may be calm the sea from on us for the sea [was] going and storming.
Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”
12 And he said to them pick up me and throw me into the sea so it may be calm the sea from on you for [am] knowing I that by which to me the storm great this [is] on you.
Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”
13 And they rowed the men to return to the dry land and not they were able for the sea [was] going and storming on them.
Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo.
14 And they called out to Yahweh and they said we beg you O Yahweh do not please let us perish by [the] life of the man this and may not you put on us blood innocent for you O Yahweh just as you pleased you have done.
Ndipo wakamlilia Bwana, “Ee Bwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umefanya kama ilivyokupendeza.”
15 And they picked up Jonah and they threw him into the sea and it stopped the sea from storming its.
Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia.
16 And they feared the men a fear great Yahweh and they sacrificed a sacrifice to Yahweh and they vowed vows.
Katika jambo hili watu wakamwogopa Bwana sana, wakamtolea Bwana dhabihu na kumwekea nadhiri.
17 And he appointed Yahweh a fish great to swallow Jonah and he was Jonah in [the] inward parts of the fish three days and three nights.
Lakini Bwana akamwandaa nyangumi kummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu, usiku na mchana.

< Jonah 1 >