< John 9 >

1 And passing by He saw a man blind from birth.
Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
2 And asked Him the disciples of Him saying; Rabbi, who sinned, this [man] or the parents of him, that blind he may be born?
Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
3 Answered (*k*) Jesus; Neither this [man] sinned nor [sinned] the parents of him, but [it was] that may be displayed the works of God in him.
Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
4 (Us *N(K)O*) it behooves to work the works of the [One who] having sent Me while day it is; is coming night, when no [one] is able to work.
Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
5 While in the world I may be, [the] light I am of the world.
Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 These things having said He spat on [the] ground and He made clay of the spittle and (he rubbed *NK(O)*) (on him *no*) the clay to the eyes (of the blind *k*)
Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
7 And He said to him; do go do wash yourself in the pool of Siloam which means Sent. He went therefore and washed and came [back] seeing.
Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
8 The therefore neighbours and those having seen him before that (a beggar *N(K)O*) he was, were saying; Surely this is the [one] sitting and begging?
Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
9 Some were saying that He it is, but others were saying; (No, *no*) (but *N(k)O*) (that *k*) like as him he is. He was saying that I myself am [he].
Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
10 They were saying therefore to him; How (then *NO*) were opened of you the eyes?
Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
11 Answered He (and said: *k*) (The *no*) man (who *no*) is being named Jesus clay made and He anointed my eyes and He said to me (that *no*) do go to (pool *k*) (*N(k)O*) Siloam and do wash. yourself Having gone (therefore *N(K)O*) and having washed I received sight.
Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
12 (And *N(k)O*) they said to him; Where is He? He says; Not I know.
Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
13 They bring him to the Pharisees who once [was] blind;
Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
14 Was now Sabbath (in which day *NO*) (when *k*) the clay made Jesus and opened of him the eyes.
Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
15 Again therefore were asking him also the Pharisees how he had received sight. And he said to them; Clay He put on my eyes and I washed and I see.
Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
16 Were saying therefore of the Pharisees some; Not is this from (*k*) God the man for the Sabbath not He does keep. Others (however *no*) were saying; How is able a man sinful such signs to do? And division there was among them.
Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
17 They say (therefore *NO*) to the blind [man] again; What you yourself say concerning Him for He opened of you the eyes? And he said that A prophet He is.
Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
18 Not did believe then the Jews concerning him that he was being blind and received sight until when they called the parents of him who having received sight,
Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
19 And they asked them saying; This is the son of you of whom you yourselves say that blind he was born? How then does he see presently
Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
20 Answered (therefore *N(k)*) (to them *k*) the parents of him and said; We know that this is the son of us and that blind he was born;
Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
21 How however presently he sees not we know, or who opened of him the eyes we ourselves not know; him do ask, (he himself *k*) [of] age is; He himself Concerning himself he will speak.
Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 These things said the parents of Him because they were afraid of the Jews; already for had agreed together the Jews that if anyone Him shall confess Christ, expelled from the synagogue he shall be.
Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
23 Because of this the parents of him said that Age he has, him (do question. *N(k)O*)
Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
24 They called therefore the man out a second time who were blind and they said to him; do give glory to God! We ourselves know that this man a sinner is.
Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
25 Answered then he (and said: *k*) Whether a sinner He is not I know; One [thing] I do know that blind being now I see.
Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
26 They said (therefore *N(k)O*) to him (again: *k*) What did He to you? How opened He of you the eyes?
Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 He answered them; I told you already, and not you did listen. Why again do you wish to hear? Surely not also you yourselves do wish His disciples to become?
Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
28 (And *n(o)*) ([they] now *o*) railed at (therefore *K*) him and said; You yourself a disciple are of that One, we ourselves however of Moses are disciples.
Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
29 We ourselves know that to Moses has spoken God, this [man] however not we know from where is.
Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
30 Answered the man and said to them; In this for (*no*) an amazing thing is that you yourselves not know from where He is, and yet (He opened *N(k)O*) my eyes.
Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
31 We know (now *k*) that to sinners God not does listen, but if anyone God-fearing shall be and the will of Him shall do, to him He listens.
Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
32 Out of the age never it has been heard that opened anyone [the] eyes of [one] blind born. (aiōn g165)
Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
33 only unless were this [man] from God, not He was able to do no [thing].
Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
34 They answered and they said to him; In sins you yourself were born entirely and you yourself teach us? And they cast him out.
Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
35 Heard (*ko*) Jesus that they had cast him out, and having found him He said (to him: *ko*) You yourself believe in the Son (of Man? *N(K)O*)
Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
36 Answered he and said; (And *no*) who is He, lord, that I may believe in Him?
Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
37 Said (now *k*) to him Jesus; Both You have seen Him, and the [One] speaking with you He is.
Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
38 And he was saying; I believe, Lord, And he worshiped Him.
Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
39 And said Jesus; For judgment I myself into world this came, that those not seeing may see and those seeing blind may become.
Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
40 (and *k*) Heard from the Pharisees these things who with Him being and they said to Him; Surely not also we ourselves blind are?
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
41 Said to them Jesus; If blind you were, not then would you have sin. since however you say that We see, the (therefore *K*) sin of you remains.
Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.

< John 9 >