< Job 5 >

1 Call please ¿ [is] there [one who] answers you and to whom? of [the] holy [ones] will you turn.
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 For a fool it slays vexation and a simple [one] it kills jealousy.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 I I have seen a fool taking root and I cursed habitation his suddenly.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 They are distant children his from safety so they may be crushed in the gate and there not [is] a deliverer.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 [the one] who Harvest his - [the] hungry he eats and to from thorns he takes it and it is eager for a snare wealth their.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 For - not it comes forth from [the] dust hardship and from [the] ground not it springs up trouble.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 For everyone to trouble he is born and [the] children of flame they make high to fly.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 But I I will seek God and to God I will set plea my.
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 [who] does Great [things] and there not [is] inquiry wonders until there not [is] number.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Who gives rain on [the] surface of [the] earth and [who] sends water on [the] surface of [the] open places.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 To set lowly [people] to a high place and mourners they are high safety.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 [who] frustrates [the] plans of Crafty [people] and not they will bring about hands their success.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 [who] catches Wise [people] when are crafty they and [the] counsel of tortuous [people] it is hasty.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 By day they meet darkness and like night they grope at noon.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 And he saved from [the] sword from mouth their and from [the] hand of [the] strong [the] needy.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 And it belonged to poor [person] hope and injustice it shuts mouth its.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 There! how blessed! [is the] person [whom] he reproves him God and [the] discipline of [the] Almighty may not you reject.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 For he he causes pain and he may bind up he shatters (and hands his *Q(K)*) they heal.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 In six troubles he will deliver you and in seven - not it will touch you harm.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 In famine he will ransom you from death and in battle from [the] hands of [the] sword.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 In [the] whip of [the] tongue you will be hidden and not you will be afraid from destruction if it will come.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 To destruction and to famine you will laugh and from [the] animal[s] of the earth may not you be afraid.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 For [will be] with [the] stones of the field covenant your and [the] animal[s] of the field it will be at peace to you.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 And you will know that [is] safety tent your and you will visit estate your and not you will miss.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 And you will know that [will be] many offspring your and descendants your [will be] like [the] vegetation of the earth.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 You will go in full strength to [the] grave as goes up a heap of sheaves at appropriate time its.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Here! this we have examined it [is] so it hear it and you know for yourself.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >