< Job 40 >
1 And he answered Yahweh Job and he said.
Bwana akamwambia Ayubu:
2 ¿ Will he contend with [the] Almighty a faultfinder [one who] corrects God let him answer him.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 And he answered Job Yahweh and he said.
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Here! I am insignificant what? will I respond to you hand my I put to mouth my.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 One [time] I have spoken and not I will answer and two [times] and not I will repeat.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 And he answered Yahweh Job (from - *Q(K)*) (a tempest *Q(k)*) and he said.
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Gird up please like a man loins your I will ask you and make known to me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 ¿ Even will you annul justice my will you condemn as guilty? me so that you may be justified.
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 And or? [does] an arm like God - [belong] to you? and with a voice like him will you thunder?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Deck yourself please majesty and dignity and glory and honor you will be clothed.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Scatter [the] furi of anger your and see every proud [person] and bring low him.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 See every proud [person] humble him and tread down wicked [people] in place their.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Hide them in the dust together faces their bind up in the hidden [place].
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 And also I I will praise you that it will save you right [hand] your.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 There! please Behemoth which I made with you grass like ox it eats.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 There! please strength its [is] in loins its and power its in [the] muscles of belly its.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 It stiffens tail its like a cedar [the] sinews of (thighs its *Q(K)*) they are intertwined.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Bones its [are] tubes of bronze limbs its [are] like a rod of iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 It [is] [the] first of [the] ways of God the [one who] made it let him bring near sword his.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 For [the] beast[s] of [the] mountains they carry to it and every animal of the field they play there.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Under thorny lotus plants it lies in a hiding place of reed[s] and swamp.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 They cover it thorny lotus plants shade its they surround it [the] poplars of [the] wadi.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 There! it is violent [the] river not it is alarmed it is confident - for it bursts forth [the] Jordan to mouth its.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 By eyes its will anyone take? it with snares will anyone pierce? a nose.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?