< Job 36 >
1 And he added Elihu and he said.
Elihu akaendelea kusema:
2 Wait for me a little so I may show you that still [are] for God words.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 I will bear knowledge my from afar (and to maker my *LAB(h)*) I will ascribe righteousness.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 For truly not [are] falsehood words my [one] complete of knowledge [is] with you.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 There! God [is] mighty and not he rejects mighty strength of heart.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Not he preserves alive [the] wicked and [the] justice of afflicted [people] he gives.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Not he withdraws from [the] righteous eyes his and with kings to the throne and he has made sit them to perpetuity and they have become exalted.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 And if [they are] bound in fetters they are caught! in cords of affliction.
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 And he told to them work their and transgressions their that they were behaving proudly.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 And he uncovered ear their for correction and he said that they will turn away! from wickedness.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 If they will hear and they may serve [him] they will bring to an end days their in good and years their in pleasant [things].
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 And if not they will hear by a missile they will pass away and they may expire like not knowledge.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 And [people] godless of heart they put anger not they cry for help if he has bound them.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 It dies in youth self their and life their among the temple prostitutes.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 He rescues [the] afflicted by affliction his and he uncovers by oppression ear their.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 And also he has allured you - from [the] mouth of enemy a broad place not constraint in place its and [the] quietness of table your it was full fatness.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 And judgment of [the] wicked you are full judgment and justice they take hold of [you].
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 For rage lest it should entice you in mockery and [the] greatness of [the] ransom may not it turn aside you.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 ¿ Will it set in order opulence your not in distress and all [the] efforts of strength.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 May not you long for the night to go up peoples in place their.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Take heed may not you turn to wickedness for this you have chosen more than affliction.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 There! God he is exalted in power his who? like him [is] a teacher.
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who? has he assigned on him way his and who? has he said you have done unrighteousness.
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Remember that you will magnify work his which they have sung people.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 All humankind they have looked on it human[s] he looks from a distance.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 There! God [is] exalted and not we know [him] [the] number of years his and not inquiry.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 For he draws up drops of water they refine rain to mist its.
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Which they flow [the] clouds they drip on - humankind numerous.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Also if anyone understands [the] spreading out of dark cloud [the] crashes of pavilion his.
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 There! he spreads out on him light his and [the] roots of the sea he covers.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 For by them he judges peoples he gives food to abundance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Over palms of hands he covers light and he commanded to it in an assailant.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 It tells on him roar his livestock also on [one who] comes up.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.