< Job 33 >

1 And but hear please O Job words my and all words my give ear to!
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Here! please I open mouth my it speaks tongue my on palate my.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 [are] [the] uprightness of Heart my words my and [the] knowledge of lips my purified they speak.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 [the] spirit of God it has made me and [the] breath of [the] Almighty it gives life me.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 If you will be able respond to me arrange! before me take your stand!
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Here! I [am] like mouth your to God from clay I was nipped off also I.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Here! dread of me not it will terrify you and pressure my on you not it will be heavy.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Surely you have spoken in ears my and [the] sound of words I heard.
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 [am] pure I not transgression [am] innocent I and not iniquity [belongs] to me.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Here! occasions on me he finds he considers me to an enemy of him.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 He puts in the stock[s] feet my he watches all paths my.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Here! this not you are in [the] right I will answer you for he is great God more than a human.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Why? against him have you contended that all words his not he answers.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 For on one [occasion] he speaks God and on two [occasions] not anyone perceives it.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 In a dream - a vision of [the] night when falls deep sleep on people in slumber on a bed.
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Then he will uncover [the] ear of people and with discipline their he will seal.
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 To turn aside a person a deed and pride from a man he will cover.
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 He will keep back life his from [the] pit and life his from passing away by missile.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 And he is chastened with pain on bed his (and [the] multitude of *Q(K)*) bones his [is] constant.
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 And it loathes it life his bread and self his food of desire.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 It wastes away flesh his from sight (and they are laid bare *Q(K)*) bones his [which] not they were seen.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 And it drew near to the pit self his and life his to [those who] bring death.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 If there on him - [is] an angel a mediator one of a thousand to tell to anyone uprightness his.
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 And he showed favor to him and he said deliver him from going down [the] pit I have found a ransom.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 It grows fresh flesh his more than youth he returns to [the] days of youth his.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 He prays to God - and he accepted him and he saw face his with a shout of joy and he restored to a person righteousness his.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 He watches - over people and he said I have sinned and upright[ness] I have perverted and not it was equal to me.
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 He has ransomed (self his *Q(K)*) from passing on in the pit (and life his *Q(K)*) on the light it will look.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Here! all these [things] he does God two times three [times] with a man.
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 To bring back self his from [the] pit to be lighted up by [the] light of life.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Pay attention O Job listen to me keep quiet and I I will speak.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 If there [are] words respond to me speak for I desire to justify you.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 If not you listen to me keep quiet and I will teach you wisdom.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >