< Job 28 >

1 For there for silver [is] a mine and a place for gold [which] people refine.
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
2 Iron from [the] dust it is taken and stone someone pours out copper.
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
3 An end - someone puts to the darkness and to every outermost part he [is] searching for [the] stone of gloom and deep darkness.
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
4 He breaks open a shaft - away from with a sojourner forgotten from foot they hang down away from humankind they swing.
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
5 [the] earth From it it comes forth food and under it it is turned over like fire.
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
6 [are] a place of Sapphire stones its and dust of gold [belong] to it.
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
7 [the] path Not it knows it a bird of prey and not it catches sight of it [the] eye of a hawk.
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
8 Not they tread it [the] sons of pride not it passes by on it a lion.
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
9 On the flint he stretches out hand his he overturns from [the] root mountains.
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
10 In the rocks shafts he splits open and every precious thing it sees eye his.
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
11 From weeping rivers he restrains and secret her he brings out light.
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
12 And wisdom from where? will it be found and where? this [is the] place of understanding.
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
13 Not he knows humankind valuation its and not it is found in [the] land of the living [ones].
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
14 [the] deep It says not [is] in me it and [the] sea it says not [it] [is] with me.
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
15 Not it will be given fine gold for it and not it will be weighed out silver price its.
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
16 Not it will be paid in [the] gold of Ophir in onyx precious and sapphire.
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
17 Not it will be comparable to it gold and glass and [is] exchange its a vessel of pure gold.
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
18 Corals and crystal not it is remembered and [the] price of wisdom [is] more than pearls.
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
19 Not it will be comparable to it topaz of Cush in gold pure not it will be paid.
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
20 And wisdom from where? does it come and where? this [is the] place of understanding.
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
21 And it has been concealed from [the] eyes of every living [thing] and from [the] bird[s] of the heavens it has been hidden.
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
22 Abaddon and death they say with ears our we have heard report its.
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
23 God he understands way its and he he knows place its.
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
24 For he to [the] ends of the earth he looks under all the heavens he sees.
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
25 To make for the wind weight and [the] waters he has measured with a measure.
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
26 When made he for the rain a decree and a path for [the] storm of thunder claps.
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
27 Then he saw it and he recounted it he established it and also he examined it.
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
28 And he said - to humankind here! [the] fear of [the] Lord that [is] wisdom and to turn from evil [is] understanding.
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”

< Job 28 >