< Job 12 >
1 And he answered Job and he said.
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Truly that you [are the] people and with you it will die wisdom.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Also [belongs] to me a heart - like you not [am] falling I more than you and with whom? [are] there not like these [things].
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 A laughingstock to friend his - I am [one who] called to God and he answered him [is] a laughingstock a righteous [person] a blameless [person].
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 [belongs] to Disaster contempt to [the] thought of [one] at ease a push [belongs] to [those who] are sliding of foot.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 They are at peace [the] tents - of destroyers and securiti [belong] to provokers of God to [those] whom he has brought God in hand his.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 And but ask please [the] animals so it may teach you and [the] bird[s] of the heavens so it may tell to you.
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Or complain to the earth so it may teach you and they may recount to you [the] fish of the sea.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Who? not does it know among all these for [the] hand of Yahweh it has done this.
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 [he] whom [is] in Hand his [the] life of every living [thing] and [the] breath of all flesh of humankind.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 ¿ Not an ear words does it test and a palate food it tastes itself.
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 [is] with Aged [people] wisdom and [is with] length of days understanding.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 [are] with Him wisdom and might [belong] to him counsel and understanding.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 There! he tears down and not it will be rebuilt he shuts on a person and not it will be opened.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 There! he holds back the waters so they may be dry and he lets loose them and they may devastate [the] earth.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 [are] with Him strength and sound wisdom [belong] to him [one who] goes astray and [one who] leads astray.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 [he is] leading away Counselors barefoot and judges he makes look foolish.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 [the] correction of Kings he loosens and he bound a loincloth on loins their.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 [he is] leading away Priests barefoot and [people] long established he overturns.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 [he is] removing A lip of trusted [ones] and [the] discernment of elders he takes away.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 [he is] pouring Contempt on noble [people] and [the] belt of strong people he loosens.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 [he is] revealing Unfathomable [things] from darkness and he brought out to the light deep darkness.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 [he is] making great the Nations and he destroyed them [he is] spreading out the nations and he led them.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 [he is] removing [the] heart of [the] leaders of [the] people of The earth and he made wander them in a wasteland not a path.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 They grope darkness and not light and he made wander them like drunkard.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.