< Jeremiah 41 >

1 And it was - in the month seventh he came Ishmael [the] son of Nethaniah [the] son of Elishama one of [the] offspring of royalty and [the] chiefs of the king and ten men [who were] with him to Gedaliah [the] son of Ahikam Mizpah towards and they were eating there food together at Mizpah.
Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
2 And he arose Ishmael [the] son of Nethaniah and [the] ten the men - who they were with him and they struck down Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan with the sword and he killed him whom he had appointed [the] king of Babylon over the land.
Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
3 And all the Jews who they were with him with Gedaliah at Mizpah and the Chaldeans who they were found there [the] men of war he struck down Ishmael.
Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
4 And it was on the day second of killing Gedaliah and anyone not he knew.
Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
5 And they came men from Shechem from Shiloh and from Samaria eighty man shaven of beard and torn of clothes and having cut themselves and an offering and frankincense in hand their to bring [the] house of Yahweh.
watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
6 And he went out Ishmael [the] son of Nethaniah to meet them from Mizpah going continually and weeping and it was when met them and he said to them come to Gedaliah [the] son of Ahikam.
Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
7 And it was when came they into [the] middle of the city and he slaughtered them Ishmael [the] son of Nethaniah into [the] middle of the cistern he and the men who [were] with him.
Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
8 And ten men they were found among them and they said to Ishmael may not you kill us for there is [belonging] to us treasures in the field wheat and barley and oil and honey and he refrained and not he killed them in among relatives their.
Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
9 And the cistern where he threw there Ishmael - all [the] corpses of the men whom he had struck down by [the] hand of Gedaliah it [was [the] one] which he had made the king Asa because of Baasha [the] king of Israel it he filled Ishmael [the] son of Nethaniah [those] slain.
Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
10 And he took captive - Ishmael all [the] rest of the people which [was] in Mizpah [the] daughters of the king and all the people who remained at Mizpah whom he had appointed Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards with Gedaliah [the] son of Ahikam and he took captive them Ishmael [the] son of Nethaniah and he went to pass over to [the] people of Ammon.
Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
11 And he heard Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies who [were] with him all the evil which he had done Ishmael [the] son of Nethaniah.
Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
12 And they took all the men and they went to do battle with Ishmael [the] son of Nethaniah and they found him to water great which [is] in Gibeon.
waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
13 And it was when saw all the people which [was] with Ishmael Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies who [were] with him and they were glad.
Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
14 And they turned round all the people which he had taken captive Ishmael from Mizpah and they turned back and they went to Johanan [the] son of Kareah.
Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
15 And Ishmael [the] son of Nethaniah he escaped with eight men from before Johanan and he went to [the] people of Ammon.
Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
16 And he took Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies who [were] with him all [the] rest of the people which he had brought back from with Ishmael [the] son of Nethaniah from Mizpah after he had struck down Gedaliah [the] son of Ahikam men [the] men of war and women and little one[s] and court-officials whom he had brought back from Gibeon.
Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
17 And they went and they remained at Geruth (Kimham *Q(K)*) which [is] beside Beth-lehem to go to go Egypt.
Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
18 From before the Chaldeans for they were afraid of them for he had struck down Ishmael [the] son of Nethaniah Gedaliah [the] son of Ahikam whom he had appointed [the] king of Babylon over the land.
ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.

< Jeremiah 41 >