< Jeremiah 34 >

1 The word which it came to Jeremiah from with Yahweh and Nebuchadnezzar [the] king of Babylon - and all army his and all [the] kingdoms of [the] earth [the] rule of hand his and all the peoples [were] fighting on Jerusalem and on all cities its saying.
Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Thus he says Yahweh [the] God of Israel go and you will say to Zedekiah [the] king of Judah and you will say to him thus he says Yahweh here I [am] about to give the city this in [the] hand of [the] king of Babylon and he will burn it with fire.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
3 And you not you will escape from hand his for certainly you will be captured and in hand his you will be given and eyes your [the] eyes of [the] king of Babylon they will see and mouth his with mouth your it will speak and Babylon you will go.
Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
4 Nevertheless hear [the] word of Yahweh O Zedekiah [the] king of Judah thus he says Yahweh on you not you will die by the sword.
“‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
5 In peace you will die and like [the] burnings of fathers your the kings former who they were before you so people will burn for you and alas! O lord they will mourn for you for a promise I I have spoken [the] utterance of Yahweh.
utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
6 And he spoke Jeremiah the prophet to Zedekiah [the] king of Judah all the words these in Jerusalem.
Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
7 And [the] army of [the] king of Babylon [were] fighting on Jerusalem and on all [the] cities of Judah which were left against Lachish and against Azekah for they they remained among [the] cities of Judah cities of fortification.
wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
8 The word which it came to Jeremiah from with Yahweh after made the king Zedekiah a covenant with all the people which [was] in Jerusalem to proclaim to them liberty.
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
9 To let go everyone [male] slave his and everyone female slave his Hebrew [masc] and Hebrew [fem] free [people] to not to work by them by a Jew brother his anyone.
Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
10 And they obeyed all the officials and all the people who they went in the covenant to let go everyone [male] slave his and everyone female slave his free [people] to not to work by them again and they obeyed and they let [them] go.
Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
11 And they turned back after thus and they took back the [male] slaves and the female slaves whom they had let go free [people] (and they subjugated them *Q(K)*) for [male] slaves and for female slaves.
Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
12 And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah from with Yahweh saying.
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
13 Thus he says Yahweh [the] God of Israel I I made a covenant with ancestors your on [the] day brought out I them from [the] land of Egypt from a house of slaves saying.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
14 From [the] end of seven years you will let go everyone brother his Hebrew who he will sell himself to you and he will serve you six years and you will let go him a free [person] from with you and not they listened ancestors your to me and not they inclined ear their.
‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
15 And you turned back you this day and you did the right in view my by proclaiming liberty everyone to neighbor his and you made a covenant before me in the house which it is called name my on it.
Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
16 And you turned back and you profaned name my and you took back everyone [male] slave his and everyone female slave his whom you had let go free [people] to desire their and you subjugated them to become of you [male] slaves and female slaves.
Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
17 Therefore thus he says Yahweh you not you have listened to me by proclaiming liberty everyone to brother his and everyone to neighbor his here I [am] about to proclaim to you liberty [the] utterance of Yahweh to the sword to pestilence and to famine and I will make you (into a terror *Q(K)*) to all [the] kingdoms of the earth.
“Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
18 And I will make the people who have transgressed covenant my who not they have carried out [the] words of the covenant which they made before me the calf which they cut into two [pieces] and they passed between pieces its.
Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
19 [the] officials of Judah and [the] officials of Jerusalem the court-officials and the priests and all [the] people of the land who passed between [the] pieces of the calf.
Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
20 And I will give them in [the] hand of enemies their and in [the] hand of [those who] seek life their and it will become corpse their food for [the] bird[s] of the heavens and for [the] animal[s] of the earth.
nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
21 And Zedekiah [the] king of Judah and officials his I will give in [the] hand of enemies their and in [the] hand of [those who] seek life their and in [the] hand of [the] army of [the] king of Babylon which have gone up from on you.
“Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
22 Here I [am] about to give command [the] utterance of Yahweh and I will bring back them to the city this and they will fight on it and they will capture it and they will burn it with fire and [the] cities of Judah I will make a waste from not inhabitant.
Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”

< Jeremiah 34 >