< Jeremiah 32 >

1 The word which it came to Jeremiah from with Yahweh (in the year *Q(K)*) tenth of Zedekiah [the] king of Judah that [was] the year eight-teen year of Nebuchadnezzar.
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza.
2 And then [the] army of [the] king of Babylon [were] laying siege on Jerusalem and Jeremiah the prophet he was shut up in [the] courtyard of the guard which [was] [the] house of [the] king of Judah.
Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.
3 Where he had shut up him Zedekiah [the] king of Judah saying why? [are] you prophesying saying thus he says Yahweh here I [am] about to give the city this in [the] hand of [the] king of Babylon and he will capture it.
Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka.
4 And Zedekiah [the] king of Judah not he will escape from [the] hand of the Chaldeans for certainly he will be given in [the] hand of [the] king of Babylon and it will speak mouth his with mouth his and eyes his (eyes his *Q(K)*) they will see.
Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe.
5 And Babylon he will take Zedekiah and there he will be until give attention to I him [the] utterance of Yahweh if you will fight with the Chaldeans not you will succeed.
Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’”
6 And he said Jeremiah it came [the] word of Yahweh to me saying.
Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
7 Here! Hanamel [the] son of Shallum uncle your [is] about to come to you saying buy for yourself field my which [is] at Anathoth for [belongs] to you [the] right of redemption to buy [it].
Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’
8 And he came to me Hanamel [the] son of uncle my according to [the] word of Yahweh to [the] courtyard of the guard and he said to me buy please field my which [is] at Anathoth which - [is] in [the] land of Benjamin for [belongs] to you [the] right of possession and [belongs] to you the redemption buy [it] for yourself and I knew that [was] [the] word of Yahweh it.
“Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’ “Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana.
9 And I bought the field from with Hanamel [the] son of uncle my which [was] at Anathoth and I weighed out! for him the silver [was] seven shekels and ten the silver.
Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba za fedha.
10 And I wrote on the document and I sealed [it] and I caused to witness [it] witnesses and I weighed out the silver on scales.
Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani.
11 And I took [the] document of the purchase the sealed [one] the order and the conditions and the uncovered [one].
Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri,
12 And I gave the document the purchase to Baruch [the] son of Neriah [the] son of Mahseiah to [the] eyes of Hanamel uncle my and to [the] eyes of the witnesses who wrote on [the] document of the purchase to [the] eyes of all the Jews who were sitting in [the] courtyard of the guard.
nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.
13 And I commanded Baruch to eyes their saying.
“Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao:
14 Thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel take the documents these [the] document of the purchase this and the sealed [one] and [the] document uncovered this and you will put them in a vessel of earthenware so that they may remain days many.
‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu.
15 For thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel again they will be bought houses and fields and vineyards in the land this.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’
16 And I prayed to Yahweh after gave I [the] document of the purchase to Baruch [the] son of Neriah saying.
“Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:
17 Alas! O Lord Yahweh there! - you you made the heavens and the earth by strength your great and by arm your outstretched not it is [too] difficult for you any thing.
“Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza.
18 [who] does Covenant loyalty to thousands and [who] pays back [the] iniquity of fathers into [the] bosom of children their after them God great mighty [is] Yahweh of hosts name his.
Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,
19 great of Counsel and [the] great of deed[s] who eyes your [are] opened on all [the] ways of [the] children of humankind to give to everyone according to ways his and according to [the] fruit of deeds his.
makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake.
20 Who you performed signs and wonders in [the] land of Egypt until the day this and in Israel and among humankind and you have made for yourself a name as the day this.
Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo.
21 And you brought out people your Israel from [the] land of Egypt by signs and by wonders and by a hand strong and by an arm outstretched and with terror great.
Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu.
22 And you gave to them the land this which you had sworn to ancestors their to give to them a land flowing of milk and honey.
Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
23 And they came and they took possession of it and not they listened to voice your (and in law your *Q(K)*) not they walked all that you had commanded to them to do not they did and you have caused to happen to them all the calamity this.
Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.
24 There! the mounds they have come the city to capture it and the city it has been given in [the] hand of the Chaldeans who are fighting on it because of the sword and the famine and the pestilence and [that] which you spoke it has happened and there you [are] seeing [it].
“Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa.
25 And you you have said to me O Lord Yahweh buy for yourself the field with silver and cause to witness [it] witnesses and the city it has been given in [the] hand of the Chaldeans.
Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’”
26 And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah saying.
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
27 Here! I [am] Yahweh [the] God of all flesh ¿ for me is it [too] difficult any thing.
“Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?
28 Therefore thus he says Yahweh here I [am] about to give the city this in [the] hand of the Chaldeans and in [the] hand of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and he will capture it.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka.
29 And they will come the Chaldeans who are fighting on the city this and they will set on fire the city this with fire and they will burn it and the houses which people made smoke on roofs their to Baal and they poured out drink offerings to gods other so as to provoke to anger me.
Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.
30 For they have been [the] people of Israel and [the] people of Judah only doing the evil in view my since youth their for [the] people of Israel only [are] provoking to anger me by [the] work of hands their [the] utterance of Yahweh.
“Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana.
31 That on anger my and on rage my it has been to me the city this from the day when they built it and until the day this to remove it from on face my.
Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu.
32 On all [the] evil of [the] people of Israel and [the] people of Judah which they have done to provoke to anger me they kings their officials their priests their and prophets their and everyone of Judah and [the] inhabitants of Jerusalem.
Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu.
33 And they turned to me a back and not a face and I taught them rising early and teaching and not they [were] listening to accept correction.
Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu.
34 And they put detestable things their in the house which it was called name my on it to make unclean it.
Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi.
35 And they built [the] high places of Baal which - [are] in [the] valley of Ben Hinnom to make pass through sons their and daughters their to Molech which not I had commanded them and not it had come up on heart my to do the abomination this so as (to cause to sin *Q(k)*) Judah.
Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.
36 And now therefore thus he says Yahweh [the] God of Israel concerning the city this which - you [are] saying it has been given in [the] hand of [the] king of Babylon by the sword and by famine and by pestilence.
“Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo:
37 Here I [will be] gathering them from all the lands where I have banished them there in anger my and in rage my and in wrath great and I will bring back them to the place this and I will cause to dwell them to security.
Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama.
38 And they will become for me a people and I I will become for them God.
Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
39 And I will give to them a heart one and a way one to fear me all the days for good for them and for children their after them.
Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.
40 And I will make to them a covenant of perpetuity which not I will turn back from after them to do good to I them and fear my I will put in heart their to not to turn aside from with me.
Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami.
41 And I will rejoice on them to do good to them and I will plant them in the land this in faithfulness with all heart my and with all being my.
Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.
42 For thus he says Yahweh just as I have brought to the people this all the calamity great this so I [will] bring on them all the good which I [am] speaking to them.
“Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi.
43 And it will be bought the field in the land this which - you [are] saying [is] a desolation it from not human being and an animal it has been given in [the] hand of the Chaldeans.
Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’
44 Fields for silver people will buy and they will write on the document - and they will seal [it] and cause to witness [it] witnesses in [the] land of Benjamin and in [the] surroundings of Jerusalem and in [the] cities of Judah and in [the] cities of the hill country and in [the] cities of the Shephelah and in [the] cities of the Negev for I will turn back captivity their [the] utterance of Yahweh.
Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao, asema Bwana.”

< Jeremiah 32 >