< Jeremiah 21 >

1 The word which it came to Jeremiah from with Yahweh when sent to him the king Zedekiah Pashhur [the] son of Malkijah and Zephaniah [the] son of Maaseiah the priest saying.
Neno lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana wakati Mfalme Sedekia alipowatuma Pashuri mwana wa Malkiya, na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwake, kusema:
2 Seek please for us Yahweh for Nebuchadnezzar [the] king of Babylon [is] waging war on us perhaps he will do Yahweh with us according to all wonders his and he may go up from on us.
“Tuulizie sasa kwa Bwana, kwa sababu Nebukadneza mfalme wa Babeli anatushambulia. Labda Bwana atatenda maajabu kwa ajili yetu kama nyakati zilizopita, ili Nebukadneza atuondokee.”
3 And he said Jeremiah to them thus you will say! to Zedekiah.
Lakini Yeremia akawajibu, “Mwambieni Sedekia,
4 Thus he says Yahweh [the] God of Israel here I [am] about to turn round [the] weapons of war which [are] in hand your which you [are] fighting by them with [the] king of Babylon and with the Chaldeans who are laying siege on you from [the] outside of the wall and I will gather them into [the] middle of the city this.
‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kuwageuzia silaha za vita zilizo mikononi mwenu, ambazo mnatumia kupigana na mfalme wa Babeli na Wakaldayo ambao wako nje ya ukuta wakiwazunguka kwa jeshi. Nami nitawakusanya ndani ya mji huu.
5 And I will fight I with you by a hand outstretched and by an arm strong and in anger and in rage and in wrath great.
Mimi mwenyewe nitapigana dhidi yenu kwa mkono wangu ulionyooshwa na mkono wa nguvu, kwa hasira na ghadhabu kali na ukali mwingi.
6 And I will strike down [the] inhabitants of the city this and the humankind and the animal[s] by a pestilence great they will die.
Nitawaangamiza waishio katika mji huu, watu na wanyama, nao watauawa kwa tauni ya kutisha.
7 And after thus [the] utterance of Yahweh I will give Zedekiah [the] king of Judah and servants his - and the people and those [who] remain in the city this from the pestilence - from the sword and from the famine in [the] hand of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and in [the] hand of enemies their and in [the] hand of [those who] seek life their and he will strike down them to [the] mouth of [the] sword not he will have mercy on them and not he will show pity and not he will have compassion.
Baada ya hayo, nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na watu wa mji huu ambao walinusurika tauni, upanga na njaa, mkononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, na kwa adui zao wale wanaotafuta uhai wao. Atawaua kwa upanga; hatakuwa na rehema juu yao au huruma wala kuwasikitikia,’ asema Bwana.
8 And to the people this you will say thus he says Yahweh here I [am] putting before you [the] way of life and [the] way of death.
“Zaidi ya hayo, waambie watu hawa, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama, naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.
9 The [one who] remains in the city this he will die by the sword and by famine and by pestilence and the [one who] goes out and he will fall on the Chaldeans who are laying siege on you (and he will live *Q(K)*) and it will belong to him life his to plunder.
Yeyote atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni. Lakini yeyote atakayetoka na kujisalimisha kwa Wakaldayo ambao wameuzunguka mji huu kwa jeshi, atanusurika, naye ataishi.
10 For I have set face my on the city this for harm and not for good [the] utterance of Yahweh in [the] hand of [the] king of Babylon it will be given and he will burn it with fire.
Nimekusudia kuufanyia mji huu jambo baya, wala si jema. Utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto, asema Bwana.’
11 And to [the] house of [the] king of Judah hear [the] word of Yahweh.
“Zaidi ya hayo, ambia nyumba ya mfalme ya Yuda, ‘Sikia neno la Bwana,
12 O house of David thus he says Yahweh judge to the morning justice and deliver [one who] has been robbed from [the] hand of an oppressor lest it should go forth like fire rage my and it will burn and there not [will be one who] extinguishes because of [the] wickedness of (deeds your. *Q(K)*)
Ewe nyumba ya Daudi, hili ndilo Bwana asemalo: “‘Hukumuni kwa haki kila asubuhi, mwokoeni mikononi mwa mdhalimu yeye aliyetekwa nyara, la sivyo ghadhabu yangu italipuka na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mlioufanya: itawaka na hakuna wa kuizima.
13 Here I [am] against you O inhabitant of the valley O rock of the plain [the] utterance of Yahweh O those [who] say who? will he come down on us and who? will he come in hiding places our.
Niko kinyume nawe, ee Yerusalemu, wewe uishiye juu ya bonde hili kwenye uwanda wa juu wa miamba, asema Bwana, wewe usemaye, “Ni nani awezaye kuja kinyume chetu? Nani ataingia mahali pa kimbilio letu?”
14 And I will visit [judgment] on you according to [the] fruit of deeds your [the] utterance of Yahweh and I will kindle a fire in forest its and it will consume all around it.
Nitawaadhibu kama istahilivyo matendo yenu, asema Bwana. Nitawasha moto katika misitu yenu ambao utateketeza kila kitu kinachowazunguka.’”

< Jeremiah 21 >