< Jeremiah 13 >

1 Thus he said Yahweh to me go and you will buy for yourself a loincloth of linen and you will put it on loins your and in water not you must cause to go it.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
2 And I bought the loincloth according to [the] word of Yahweh and I put [it] on loins my.
Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
3 And it came [the] word of Yahweh to me a second [time] saying.
Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
4 Take the loincloth which you bought which [is] on loins your and arise go Perath towards and hide it there in [the] cleft of the rock.
“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
5 And I went and I hid it at Perath just as he had commanded Yahweh me.
Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
6 And it was from [the] end of days many and he said Yahweh to me arise go Perath towards and take from there the loincloth which I commanded you to hide it there.
Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
7 And I went Perath towards and I dug and I took the loincloth from the place where I had hidden it there and there! it was ruined the loincloth not it was profitable for anything.
Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
8 And it came [the] word of Yahweh to me saying.
Ndipo neno la Bwana likanijia:
9 Thus he says Yahweh thus I will ruin [the] pride of Judah and [the] pride of Jerusalem great.
“Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 The people this wicked who are refusing - to hear words my who walk in [the] stubbornness of own heart their and they have walked after gods other to serve them and to bow down to them and let it be like the loincloth this which not it is profitable for anything.
Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
11 For just as it clings loincloth to [the] loins of a person so I have made cling to me all [the] house of Israel and all [the] house of Judah [the] utterance of Yahweh to become for me a people and a name and praise and honor and not they listened.
Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
12 And you will speak to them the word this. Thus he says Yahweh [the] God of Israel every wineskin it will be filled wine and they will say to you ¿ really not do we know that every wineskin it will be filled wine.
“Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
13 And you will say to them thus he says Yahweh here I [am] about to fill all [the] inhabitants of the land this and the kings who sit for David on throne his and the priests and the prophets and all [the] inhabitants of Jerusalem drunkenness.
Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
14 And I will smash them each to brother his and the parents and the children alike [the] utterance of Yahweh not I will show pity and not I will have mercy and not I will have compassion from destroying them.
Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
15 Hear and give ear may not you be haughty for Yahweh he has spoken.
Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
16 Give to Yahweh God your glory before he will bring darkness and before they will stumble feet your on mountains of twilight and you will wait for light and he will make it into deep darkness (and he will make [it] *Q(K)*) into thick darkness.
Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
17 And if not you will listen to it in secret places it will weep self my because of pride and utterly it will weep and it may run down eye my tear[s] for it has been taken captive [the] flock of Yahweh.
Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
18 Say to the king and to the queen-mother make low sit for it has come down [the] place of head your [the] crown of splendor your.
Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
19 [the] cities of The Negev they have been shut up and there not [is one who] opens it has been taken into exile Judah all of it it has been taken into exile completeness.
Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
20 (Lift up *Q(K)*) eyes your (and see *Q(K)*) those [who] are coming from [the] north where? [is] the flock [which] it was given to you [the] sheep of beauty your.
Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
21 What? will you say that he will appoint over you and you you taught them over you close friends to chief ¿ not labor-pains will they seize you like a woman giving birth.
Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
22 And if you will say in heart your why? have they happened to me these [things] in [the] greatness of iniquity your they have been uncovered skirts your they have suffered violence heels your.
Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
23 ¿ Will he change a Cushite skin his and a leopard spots its also you you will be able to do good O [those] trained to do evil.
Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
24 And I will scatter them like chaff [which] passes away to [the] wind of [the] wilderness.
“Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
25 This [is] lot your [the] portion of measure your from with me [the] utterance of Yahweh that you have forgotten me and you have trusted in falsehood.
Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 And also I I will strip off skirts your on face your and it will be visible shame your.
Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
27 Adulteri your and neighings your [the] wickedness of prostitution your on hills in the field I have seen detestable things your woe! to you O Jerusalem not you are clean after when? yet.
uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”

< Jeremiah 13 >