< Isaiah 46 >

1 He has bowed down Bel [is] stooping low Nebo they belong idols their to the animal[s] and to the cattle burdens your [are] carried a load for a weary [animal].
Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
2 They have stooped low they have bowed down together not they have been able to rescue a burden and self their in captivity it has gone.
Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
3 Listen to me O house of Jacob and all [the] remnant of [the] house of Israel who have been carried from [the] belly who have been borne from [the] womb.
“Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
4 And until old age I [am] he and until gray hair I I will carry I I made and I I will bear and I I will carry and I may rescue.
Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
5 To whom? will you liken me and you may make [me] equal? and will you compare? me and we may be alike.
“Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
6 Those [who] pour out gold from a bag and silver on scale[s] they weigh out they hire a metalsmith and he makes it a god they prostrate themselves also they bow down.
Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
7 They lift up it on a shoulder they carry it and they set down it in place its so it may stand from place its not it departs also he cries out to it and not it answers from trouble his not it delivers him.
Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
8 Remember this and pluck up courage bring [it] back O rebels on heart.
“Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
9 Remember former [things] from long ago for I [am] God and there not [is] yet God and there not [is] like me.
Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
10 [one who] declares From [the] beginning [the] end and from antiquity [things] which not they have been done [one who] says purpose my it will be fulfilled and all desire my I will accomplish.
Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
11 [one who] calls From [the] east a bird of prey from a land of distance a man of (purpose my *Q(K)*) also I have spoken also I will bring it I have planned also I will accomplish it.
Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
12 Listen to me O [people] mighty of heart O [people] distant from righteousness.
Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
13 I have brought near righteousness my not it is far away and salvation my not it will delay and I will give in Zion salvation to Israel splendor my.
Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.

< Isaiah 46 >